Mwaka mpya: Hivi ndivyo dunia ilivyoupokea mwaka 2022, huku ikikabiliwa na maambukizi ya omicron

Fataki ziliukaribisha mwaka 2022 mjini London

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Fataki ziliukaribisha mwaka 2022 mjini London

Mamilioni ya watu walishuhudia fataki za mwaka mpya katika miji tofauti duniani,huku dunia ikishuhudia wimbi jipya la maambukizi ya aina mpya ya virusi vya corona katika linaloyakumba baadhi ya maeneo yake.

La imagen de un león creada con drones en el cielo de Londres.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Picha ya simba iliyobuniwa na droni katika anga la mji wa London

Fuegos artificiales en la Puerta de Brandenburgo, Berlín.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Lango la Brandenburg mjini Berlin Ujerumani lilikuwa ni moja ya maeneo muhimu duniani yaliyoukaribishwa mwaka mpya kwa milio ya fataki.

Sherehe hatahivyo ziliendelea, kuwa tofauti katika naadhi ya maeneo kutokana na janga la Covid-19, ambalo tangu mwaka 2020 limezilazimisha serikali kuweka sheria na masharti ili kuepuka mikusanyiko ya umati wa watu.

Fuegos artificiales sobre la Acrópolis en Atenas, Grecia.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Fataki juu ya Acropolis katika Athens, Ugiriki, kuadhimisha kuwasili kwa mwaka 2022

Moja ya nchi za kwanza dunaini kuukaribisha mwaka 2022 ilikuwa ni Australia , ambako fataki zilitawa anga juu ya bandari ya Sydney ya Jackson Bay.

Fuegos artificiales en Sídney, Australia.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Fataki katika Sydney, Australia, juu ya bandari ya Port Jackson Bay

Licha a janga, tabasamu za watu ziliweza kushuhudiwa katika picha za tukio.

Personas en las calles de la ciudad de Melboure, en Australia, reciben el Año Nuevo

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Nchini Australia baadhi ya watu waliingia mitaani, pamoja na jiji la Melboure.

Kinyume na Australia, New Zealand iliukaribisha mwaka mpya kwa mataa na kuepuka fataki, tukio hilo lilifanyika Auckland, kutoka kwenye mnara wa Skytower.

Espectáculo de luces en Auckland, capital de Nueva Zelanda.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Onyesho la mataa katika Auckland, mji mkuu wa New Zealand.

Katika Taiwan kulikuwa na onyesho la fataki katika wilaya ya Xinyi Taipei. Sawa na Australia, watu pia waliruhusiwa kukusanyika kushuhudia tukio hilo.

Fuegos artificiales en Taipei, capital de Taiwán.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Fataki katika Taipei, mji mkuu wa Taiwan.

Wakati huo huo katika mji wa Tokyo, furaha ilitawala mitaa. Watu walikusanyika kuukaribisha mwaka pya, hususan katika mji wa Shibuya, huku wakiwa wamevalia mavazi ya rangi za kuvutia, wakitabasamu na kulikuwa na polisi wengi.

Mwaka mpya ulikaribishwa huku kukiwa na wimbi la wasi wasi, huku kukiwa na watu waliopatikana na aina moya ya kirusi cha omicron , ambacho kinasambaa kwa kasi kubwa zaidi kote duniani.

Un hombre con ropa de luces recibe el 2022 en las calles de Tokio, Japón

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Katika Japan, watu waliingia mitaani na kuukaribisha mwak 2022 kwa mavazi ya rangi za kuvutia na uwepo mkubwa wa polisi

Kufikia Alhamisi visa vipya, 1,944,392 vya virus viliripotiwa duniani

Personas conglomeradas en las calles de Japón durante la celebración de Año Nuevo. Un hombre lleva un traje de Pikachu

Chanzo cha picha, Yuichi Yamazaki

Serikali nyingi zinahofia kwamba kuongezeka kwa maambukizi kunaweza kuzidi uwezo wa hospitali, ingawa matokeo ya tafiti za awali yanaonyesha kirusi cha Omicron kina adhari ndogo kuliko vilivyotangulia.

Wakati mwamka 2022 ulipoingia, eneo maarufu la Red Square mjini Moscow lilikuwa pweke, kinyume na kawaida yake.

Kutokana na janga la corona, sherehe zilizozoweleka katika medani hiyo maarufu zilifutwa, lakini halikupungukiwa fataki.

Plaza Roja de Moscú sin público, pero iluminada con los juegos artificiales.

Chanzo cha picha, EPA/MAXIM SHIPENKOV

Maelezo ya picha, Medani ya Moscow Red Square bila hadhira.

Eneo la the Big Apple liliukaribishwa mwaka kwa miziki ya aina mbali mbali , mataa, na itifaki ya usalama kwa wale waliofika kwenye sherehe maarufu katika eneo la Times Square: wakiwa wamepata chanjo kamili na wamevalia barakoa.

Times Square

Chanzo cha picha, REUTERS/Dieu-Nalio Chery

Maelezo ya picha, Sherehe ya mwaka mpya katika eneo la Times Square.

Iingawa kulikuwa na watu wachache , kutokana na kuogezeka kwa maambukizi ya COVID-19 katika mji wa New York, sherehe ya kuukaribisha mwaka mpya ilijumuisha onyesho la muziki.

Los cantantes Ja Rule and Ashanti animaron las celebraciones en Nueva York.

Chanzo cha picha, REUTERS/Hannah Beier

Maelezo ya picha, Waimbaji Ja Rule na Ashanti wakitumbuiza katika sherehe za mwaka mpya katika mji wa New York.

Pia Rio de Janeiro iliukaribisha mwaka mpya kwa fataki katika ufukwe wa Copacabana, licha ya kwamba watu walikuwa ni wachache kutoka na janga la Corona.

Playa de Copacabana

Chanzo cha picha, REUTERS/Ricardo Moraes

Maelezo ya picha, Copacabana beach