Coronavirus: Idadi ya waliopoteza maisha yafikia 366, kutoka 133

Chanzo cha picha, EPA
Idadi ya watu waliopoteza maisha kutokana na virusi vya corona nchini Italia imeongezeka kutoka 133 na kufikia 366 kwa siku moja, maafisa wameeleza.
Maambukizi yameongezeka kwa asilimia 25% na kufikia 7,375 kutoka 5,883 kwa mujibu wa shirika la kitaifa la utabiri na udhibiti wa matukio ya dharura.
Ongezeko la maambukizi limekuja wakati mamilioni ya watu wakichukua hatua zilizotangazwa siku ya Jumapili ili kudhibiti maambukizi.
Watu takribani milioni 26 mjini Lombardy na katika majimbo 14 chini ya sheria mpya ya karantini wanahitaji ruhusa maalum kusafiri.
Waziri Mkuu Giuseppe Conte pia ametangaza kufugwa kwa shule, maeneo ya kufanya mazoezi, makumbusho, nyumba za starehe na maeneo mengine yanayokusanya watu wengi.
Mazuio hayo yatadumu mpaka tarehe 3 mwezi Aprili.

Chanzo cha picha, Getty Images
Ongezeko hili linamaanisha kuwa Italia kwa sasa ina idadi kubwa iliyothibitishwa nje ya China, ambapo mlipuko ulianzia mwezi Desemba. Idadi hii imezidi Korea Kusini, ambayo ina idadi ya maambukizi 7,313.
Italia ni nchi mojawapo duniani yenye idadi kubwa ya watu wenye umri mkubwa. Virusi ni hatari sana hasa kwa wazee.
Miongoni mwa watu waliopata maambukizi hivi karibuni ni mkuu wa jeshi. Salvatore Farina alisema alijisikia vizuri na alijitenga mwenyewe kuepuka kuambukiza wengine.
Taratibu mpya za karantini zinaathiri robo ya raia wa Italia na katikati mwa mji tajiri ulio kaskazini mwa nchi hiyo ambao ni chachu ya uchumi wa nchi hiyo.
Mfumo wa afya ni changamoto mjini Lombardy, mji ulio kaskazini mwa nchi hiyo wenye watu milioni 10. Watu wamekuwa wakitibiwa kwenye kumbi za hospitali.
''Tunataka kuhakikisha afya njema kwa raia wetu. Tunaelewa kuwa hatua hizi zinahitaji kujitoa, wakati mwingine kidogo wakati mwingine kujitoa kwa kiasi kikubwa,'' Waziri Mkuu Conte alisema wakati akitangaza hatua hizo mpya.
Chini ya hatua mpya, watu hawapaswi kuingia au kutoka Lombardy.
Hatua hizo hizo zinachukuliwa Modena, Parma, Piacenza, Reggio Emilia, Rimini, Pesaro and Urbino, Alessandria, Asti, Novara, Verbano Cusio Ossola, Vercelli, Padua, Treviso and Venice.
Idara ya mambo ya Uingereza imeshauri kutosafiri bila sababu ya lazima kuelekea maeneo hayo.

Mkuu wa Shirika la Afya duniani, WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus ameisifu Italia kwa ''kujitoa kwao kwa dhati'' kwa kuweka mazuio. Mpaka siku ya Jumapili karibu watu 50,000 Kaskazini mwa Italia waliathirika na karantini.
Juma lililopita serikali ilitangaza kufungwa kwa shule zote na vyuo nchi nzima kwa siku 10.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe
Hali ikoje maeneo mengine duniani?
Idadi ya maambukizi ulimwenguni ni zaidi ya 107,000, na vifo vipatavyo 3,600.
Athari kubwa imeonekana nchini China. Lakini siku ya Jumapili iliripoti idadi ya chini zaidi ya maambukizI mapya katika siku moja tangu Januari - ishara kwamba kuenea kwa virusi kunapungua.
Iran, moja ya maeneo yenye maambukizi mabaya zaidi nje ya China, sasa imethibitisha maambukizi 6,566 na vifo 194.
Hatahivyo, takwimu halisi zinakisiwa kuwa za juu zaidi. Ripoti moja Jumapili, ikinukuu mjumbe wa serikali, ikisema kulikuwa na vifo 200 katika mkoa wa kaskazini wa Gilan pekee - lakini takwimu hizo baadaye ziliondolewa.
Huko Ufaransa, virusi vinaenea miongoni mwa wabunge. Wabunge wawili walikutwa na maambukizi, maafisa walieleza siku ya Jumapili.
Kwa jumla manaibu wanne wameambukizwa. Pia Jumapili Ufaransa iliripoti visa 1,126, ongezeko la 19% kwa siku na idadi kubwa ya maambukizi barani Ulaya baada ya Italia.
Serikali ya Ufaransa imepiga marufuku mikusanyiko ya watu zaidi ya 1,000.
Nchini Marekani, zaidi ya watu 470 wamekutwa na maambukizi ya Covid-19 na mpaka sasa waliopoteza maisha ni watu 21.
Miongoni mwa nchi zilizoripoti ongezeko la maambukizi ni Ujerumani 939, Uhispani 589, Uingereza 273 na Uholanzo 265.
Albania, Bulgaria, Colombia, Costa Rica, visiwa vya Maldives, Malta, na Paraguay zimeripoti visa vya kwanza vya maambukizi ya virusi hivyo.














