Moja kwa moja, Sitairuhusu Iran kuwa na silaha za nyuklia – Trump

Rais wa Marekani amesema: "Kwa miongo kadhaa, imekuwa sera ya Marekani kutoruhusu Iran kupata silaha za nyuklia.”

Moja kwa moja

Rashid Abdallah

  1. Sitairuhusu Iran kuwa na silaha za nyuklia – Trump

    ll

    Chanzo cha picha, Reuters

    Rais wa Marekani Donald Trump ametoa hotuba yake ya kila mwaka katika majengo ya Bunge la Marekani na kusisitiza kuwa hatoiruhusu Iran kuwa na silaha za nyuklia.

    Rais wa Marekani amesema: "Kwa miongo kadhaa, imekuwa sera ya Marekani kutoruhusu Iran kupata silaha za nyuklia.”

    “Wameonywa wasijaribu kujenga upya mpango wao wa silaha, lakini wanaendelea kufuata matarajio yao mabaya ya nyuklia. Napenda tutatue tatizo hili kupitia diplomasia, lakini jambo moja ni hakika: Sitawaruhusu kupata silaha za nyuklia."

    Trump ameweka rekodi ya hotuba ndefu zaidi, akitumia karibu saa 1 na dakika 50, akiizidi rekodi ya Bill Clinton ya hotuba yake ya mwisho mnamo 2000.

  2. 'Iwapo Marekani itafanya makosa ya kutushambulia itapata hasara kubwa' - Mkuu wa Jeshi Iran

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Mkuu wa Jeshi la Iran Jenerali Mousavi

    Hapo awali tuliripoti kwamba Waziri wa Ulinzi wa Armenia Soren Papikyan alisafiri hadi Tehran na kukutana na Waziri wa Ulinzi wa Irani Aziz Nasirzadeh.

    Meja Jenerali Abdolrahim Mousavi, Mkuu wa Jeshi la Iran pia alikutana naye.

    Bwana Mousavi alisema katika mkutano huo: "Sisi hatukuwa waanzilishi wa vita vyovyote, na mbinu yetu huko nyuma ilikuwa kuzuia kupanuka kwa wigo wa vita na kupunguza majeruha. Lakini hatua za Marekani zilitufanya kubadili mtazamo wetu, na wakati huu, ikiwa itafanya makosa, tutaisababishia hasara kubwa."

    Msemaji wa Ikulu ya White House Carolyn Leavitt amesema leo kuwa chaguo la kwanza la Donald Trump siku zote ni diplomasia, lakini yuko tayari kutumia nguvu ikibidi.

  3. Nigeria yakana ripoti kwamba ililipa fidia ili wanafunzi waliotekwa nyara waachiliwe huru

    p;

    Chanzo cha picha, EPA/Shutterstock

    Maelezo ya picha, Zaidi ya wanafunzi 200 na wafanyakazi walichukuliwa na watu wenye silaha kutoka Shule ya St Mary's mwezi Novemba - wote waliachiliwa huru kufikia Krismasi

    Serikali ya Nigeria imekataa ripoti ya vyombo vya habari inayodai kwamba ililipa fidia kwa wanamgambo wa Kiislamu wa Boko Haram ili kuachiliwa huru kwa zaidi ya wanafunzi 200 na wafanyakazi waliotekwa nyara katika shule ya bweni ya Kikatoliki mwezi Novemba.

    Waziri wa Habari Mohammed Idris amesema madai hayo, yaliyotolewa na shirika la habari la AFP akinukuu vyanzo vya kijasusi, kuwa "ya uwongo na yasiyo na msingi."

    Pia amekanusha kwamba makamanda wawili wa Boko Haram waliachiliwa huru kama sehemu ya makubaliano hayo.

    Nigeria inakabiliwa na tatizo la utekaji nyara - huku wahalifu wakiwa ni pamoja na wanamgambo wa Kiislamu, wanachama wa magenge yanayojulikana kama "majambazi" na watu wanaotaka kujitenga.

    Baadhi ya wachambuzi walionukuliwa na AFP wanaamini utekaji nyara katika Shule ya St Mary huko Papiri katika jimbo la magharibi mwa Niger uliongozwa na kamanda maarufu wa wanamgambo wa Boko Haram anayejulikana kama "Sadiku."

    Ingawa Boko Haram inasalia kuwa na shughuli nyingi zaidi katika jimbo la Borno kaskazini-mashariki, ambapo kundi hilo lilianza uasi wake mwaka 2009, mitandao mingine ya uhalifu ina shughuli katika sehemu kubwa za maeneo ya kaskazini-magharibi na kaskazini-kati mwa Nigeria.

    Chanzo kimoja kilichonukuliwa na AFP kilidai fidia hiyo ilifikia takriban naira milioni 40 (karibu dola 30,000, pauni 22,000) kwa kila mateka, huku chanzo kingine kikidokeza kwamba jumla ya naira bilioni 2 (karibu dola milioni 1.5) zililipwa.

    Ripoti hiyo pia ilidai pesa hizo zilisafirishwa kwa ndege hadi kwenye eneo la Gwoza la Boko Haram katika jimbo la Borno na kukabidhiwa kwa kamanda wa eneo hilo.

    "Madai kwamba fidia ilitolewa kwa helikopta kwa waasi, pamoja na uthibitisho wa risiti kuvuka mpaka, ni hadithi ya kubuni," Idris alisema katika taarifa hiyo.

    Boko Haram walipata umaarufu mwaka wa 2014 kwa kuwateka nyara zaidi ya wasichana 200 wa shule kutoka kijiji cha Chibok.

    Tangu wakati huo nchi imekabiliwa na ongezeko la utekaji nyara kwa wingi, huku wachambuzi wakisema kwamba malipo ya fidia - kutoka kwa familia, wapatanishi au, katika baadhi ya matukio, mamlaka za serikali - yamesaidia kuchochea kile ambacho baadhi hukielezea kama "sekta ya utekaji nyara kwa faida".

  4. Mexico yawasaka wafungwa 23 waliotoroka gerezani wakati wa vurugu

    p

    Chanzo cha picha, EPA

    Polisi nchini Mexico inawasaka wafungwa kadhaa waliotoka gerezani huko Puerto Vallarta wakati wa wimbi la machafuko yaliyoanzishwa na genge la dawa za kulevya la Jalisco New Generation Cartel (CJNG) siku ya Jumapili.

    CJGN ilifanya vurugu kulipiza kisasi kwa mauaji ya kiongozi wao, Nemesio Oseguera Cervantes, anayejulikana kama "El Mencho" na vikosi vya usalama.

    Wakati wa machafuko hayo, watu wenye silaha waligonga milango ya gereza kwa gari, na kuwafungulia njia wafungwa 23 kutoroka, amesema afisa mmoja.

    Zaidi ya watu 70 - wakiwemo wanajeshi 25 - waliuawa katika operesheni ya kukamata El Mencho na vurugu zilizofuata.

    Pia unaweza kusoma:

  5. Hujambo na karibu

    Nakukaribisha katika taarifa zetu za moja kwa moja, leo Jumatano tarehe 25/2/2025