Jordan imezindua makavazi ya kwanza ya kijeshi chini ya bahari

Chanzo cha picha, AFP
Jordan imezindua makavazi yake ya kwanza ya kijeshi chini ya bahari katika pwani ya Aqaba.
Katika hafla ya uzinduzi huo siku ya Jumatano, ufalme huo ulizamisha magari kadhaa ya kivita pamoja na helikopta kijeshi chi ya bahari.
Magari hayo yameegeshwa kana kwamba yako vitani yamewekwa katika miamba ya matumbawe yaliopo chini ya bahari nyekundu.
Mamlaka zinasema onyesho hilo ni mbinu mpya ya utalii kwa wageni wanaozuru taifa hilo.
Miamba ya matumbawe katika sehemu ya Kaskazini mwa Bahari nyekundu ni kivutio kikubwa kwa wapiga mbizi na watalii wengine.
Halmashauri ya eneo maalum la kiuchumi la Aqaba (ASEZA) imeongeza kuwa itajumuisha aina tofauti ya michezo katika "mazingira hayo ya maonesho".

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, Reuters
Picha zotye zina haki miliki.








