Wimbo mpya wa Diamond unaomshirikisha Zari 'Iyena' wazua hisia

Nyota wa muziki wa bongo nchini Tanzania DIamond Platinumz

Chanzo cha picha, AFP/Getty Images

Maelezo ya picha, Nyota wa muziki wa bongo nchini Tanzania DIamond Platinumz
Muda wa kusoma: Dakika 2

Wimbo mpya wa nyota wa muziki wa bongo Diamond Platinumz kwa jina 'Iyena' unaomshirikisha mfanyibiashara wa Uganda na mama wa watoto wake wawili Zari Hassan umezua hisia kali.

Wimbo huo ambao ni wa pili katika albamu yake ya ABoyFromTandale kwa jina IYENA unaomuhusisha msanii Rayvanny unamuonyesha mwanamuziki huyo akifunga ndoa na Zari Hassan licha ya wawili hao kuwachana.

Kanda hiyo ya video ilio na mandhari ya ndoa ilirekodiwa wakati wawili hao walipokuwa pamoja.

Katika wimbo huo Platinumz anaonekana akifunga ndoa na mama wa watoto wake wawili huku Rayvany na Fahyma wakiwa wasimamizi wakuu wa harusi hiyo.

Baadhi ya mashabiki walidhania kwamba wimbo huo ulikuwa wa ishara ya msani huyo kurudiana na Zari Hassan

Ruka X ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 1

Katika wimbo huo Platinumz anamuhakikishia Zari kwamba 'talaka ndio njia ya mwisho atakayokuwa akifikiria baada ya kufunga ndoa'.

Mfanyibiashara na raia wa Uganda Zari Hassan
Maelezo ya picha, Mfanyibiashara na raia wa Uganda Zari Hassan

Hivi ndivyo msanii huyo alivyoandika katika mtandao wake wa twitter kabla ya kutoa kibao hicho:

Ruka X ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 2

Na punde tu baadaye mashabiki wake walituma ujumbe katika mtadao wa twitter wakijibu.

Ruka X ujumbe, 3
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 3

Hatahivyo kuna wale waliokerwa na msanii huyo kutoa wimbo huo mwezi mtukufu wa Ramadhan

Ruka X ujumbe, 4
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 4

Ruka X ujumbe, 5
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 5

Zari na Diamond waliwachana mwezi Februari mwaka huu baada ya kuwa pamoja kwa takriban miaka mitatu.

Zari alisitisha uhusiano wao siku ya wapendwanao ya Valentine kwa kuchapisha ua jeusi na ujumbe mrefu kwa Diamond akisema amechoshwa na 'tabia' ya mwanamuziki huyo.