Harusi ya Kifalme ya Prince Harry na Meghan Markle: Mwanamfalme Harry na Meghan wafunganishwa katika ndoa Windsor Castle

harry and meghan kiss

Chanzo cha picha, PA

Muda wa kusoma: Dakika 3

Bi Meghan Markle na Mwanamfalme Harry wamevishana pete na kutangazwa kuwa mume na mke Windsor Castle katika sherehe inayofuatiliwa na mamilioni ya watu kupitia runinga, mtandao na redio.

Wawili hao walifunganishwa katika ndoa mbele ya Malkia na wageni 600 waliokuwemo ndani ya kanisa la St George, katika Windsor Castle.

Bi Markle alikuwa amevalia vazi la harusi lililoshonwa na fundi mbunifu wa mitindo Mwingereza Clare Waight Keller.

Bi Meghan alitumia gari aina ya Rolls Royce Phantom kufika kanisani ambapo alipokelewa kwa shangwe na nderemo aliposhuka kutoka kwenye gari hilo na kuingia kanisa la St George.

Miongoni mwa wageni waliofika ni nyota wa televisheni Marekani Oprah Winfrey na mwigizaji Idris Elba.

George na Amal Clooney, David na Victoria Beckham pamoja na Elton John pia wamewasili.

Mwanamfalme Harry na Meghan Markle baadaye walipitia kwenye mji wa Windsor kwa msafara kwa kutumia kigari maalum cha kuvutwa na farasi.

Maelezo ya video, Mwanamfalme Harry akimfunua Meghan Markle wakati wa harusi yao

Mwanamfalme Harry amepewa cheo cha Mtawala wa Sussex na bibi yake Malkia Elizabeth II, naye Bi Markle sasa atakuwa Mke wa Mtawala wa Sussex.

Mwanamfalme Harry, ambaye ni wa sita kwenye orodha ya warithi wa ufalme, pia amepokezwa vyeo vya Earl wa Dumbarton na Baron Kilkeel.

Meghan
Meghan na Harry exchange vows

Chanzo cha picha, PA

Maelezo ya picha, Meghan na Harry wakitangazwa kuwa mume na mke
Prince Harry and Meghan Markle in St George"s Chapel at Windsor Castle

Chanzo cha picha, PA

Maelezo ya picha, Mwanamfalme Harry na Meghan Markle katika kanisa la St George, Windsor Castle
Wawili hao wakiwa wameketi kanisani

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Wawili hao wakiwa wameketi kanisani
meghan markle dress
Prince Charles walked Ms Markle down the aisle
Maelezo ya picha, Mwanamfalme Charles (babake Prince Harry) akimsindikiza Bi Markle kumpeleka kwenye madhabahu

Maelfu ya watu wamefika Windsor kufuatilia harusi hiyo, wengi walikesha kuhakikisha wanapata nafasi nzuri ya kujionea yaliyokuwa yanajiri.

Princes Harry and William

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Mwanamfalme Harry na msimamizi wake kwenye harusi, kakake Mwanamfalme William
David Beckkam and the Clooneys

Chanzo cha picha, PA

Maelezo ya picha, David Beckkam na George na Amal Clooney

Mwanamfalme Charles, babake Mwanamfalme Harry, ndiye aliyeyemsindikiza Bi Markel kwenda kwenye madhabahu baada ya babake Thomas kushindwa kuhudhuria harusi hiyo kutokana na sababu za kiafya.

Mkesha wa harusi, Mwanamfalme Harry, 33, aliambia umati wa watu Windsor kwamba anajihisi "mtulivu" na kwamba Bi Markle, 36, anajihisi "vyema sana".

Katika kiapo chake cha ndoa, Bi Markle hakuahidi "kumtii" mume wake. Mwanamfalme Harry ameamua kuwa na pete ya ndoa.

Meghan's mother, Doria Ragland

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mamake Meghan, Doria Ragland, ndiye jamaa pekee wa Bi Markle aliyehudhuria sherehe hiyo
US TV star Oprah Winfrey, wearing pink, and British actor Idris Elba arrive at the chapel

Chanzo cha picha, PA

Maelezo ya picha, Oprah Winfrey (mwenye vazi la waridi) na mwigizaji Idris Elba wakiwasili kwa sherehe

Wageni 600 walifuatilia harusi hiyo, ambayo iliongozwa na Askofu Mkuu wa Canterbury, Justin Welby, katika kanisa la St George.

Women wear wedding dresses on the Long Walk

Chanzo cha picha, PA

Maelezo ya picha, Baadhi ya waliofika kutazama harusi hiyo wamevalia mahsusi
Royal fans arrive at train station

Chanzo cha picha, PA

Maelezo ya picha, Wengi walifika Windsor asubuhi na mapema Jumamosi
Presentational grey line
Flowers and foliage surround the West Door and steps of St George's Chapel at Windsor Castle

Chanzo cha picha, PA

Maelezo ya picha, Mlango wa Magharibi, na vidato vya kanisa la St George vyote vimepambwa kwa maua na majani
Flowers adorn the front of the organ loft inside St George"s Chapel at Windsor Castle

Chanzo cha picha, PA

Maelezo ya picha, Hata ndani ya kanisa, mambo ni vivyo hivyo
Maelezo ya video, Prince Harry na Markle: Mtanzania aliyetoka Cardiff kufika kwa harusi Windsor

Umati wa watu wakiungana na waandishi wa habari kutoka maeneo mengi duniani wamlikusanyika Windsor kwa sherehe hii kubwa.

Inakadiriwa kwamba watu hadi 100,000 walikuwa kwenye barabara za mji huo.

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe

Grace Gothard
Maelezo ya picha, Grace Gothard kutoka London alisema alikuwa furaha sana kuhudhuria harusi hiyo
Janet Butterfield and Ray Brown
Maelezo ya picha, Janet Butterfield na Ray Brown kutoka Bradford, Yorkshire wanasema harusi ya sasa inavutia zaidi kuliko ya Mwanamfalme William na Kate

Watu wa kawaida 1,200, wengi ambao wametambuliwa kwa juhudi zao za hisani katika jamii, walialikwa kuhudhuria harusi hiyo Windsor Castle.

Meghan Markle and Doria Ragland

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Doria Ragland alikuwa ndiye pekee kutoka familia ya Markle aliyehudhuria sherehe hiyo

Bi Markle alikuwa na mabinti 10 wapamba harusi na wavulana, wote wa chini ya miaka minane, wakiwemo Mwanamfalme George na Bintimfalme Charlotte.

Bi harusi alilakiwa na Mwanamfalme Charles, ambaye alimtembeza hadi kwenye madhabahu.

Wakati wa ibada, wawili hao walikula kiapo kila mmoja akijitoa kwa mwenzake na kusema: "kwa mema, kwa mabaya, kwa ujatajiri, kwa umaskini, kwa ugonjwa na kwa afya, kukupenda na kukuenzi, tangu kifo kitutenganishe."

Royal wedding fans

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Wawili hawa walikesha Windsor
Karen Gibson and The Kingdom Choir

Chanzo cha picha, PA

Maelezo ya picha, Karen Gibson na kwaya yake ya Kingdom Choir ni miongoni mwa waliotumbuiza