Mwalimu aliyefundisha kompyuta ubaoni aalikwa na Microsoft

Muda wa kusoma: Dakika 1

Je, unakumbuka picha za mwalimu huyu,Owura Kwadwo.

Mafunzo ya kompyuta bila kwa njia ya ubao

Chanzo cha picha, INNOCENT FRIMPONG

Maelezo ya picha, Mafunzo ya kompyuta bila kwa njia ya ubao

Mwezi uliopita mwalimu huyu alivuma mtandaoni baada ya kuweka picha akichora programu ya Microsoft Word kwenye ubao wakati wa darasa la tarakilishi.

Iligundulika kwamba alifanya hivyo kwa sababu shule anayofundishia haikuwa na tarakilishi za kuwafundushia wanafunzi somo hilo la kompyuta.

Alisema "kufundisha somo la kompyuta nchini Ghana inachekesha.

Sasa mwalimu huyo anahudhuria mkutano wa walelimishaji wa Microsoft unaofanyikia nchini Singapore.

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe

Ameandika katika ukurasa wake wa Facebook, "Nimefika nchini Singapore katika mkutani wa Microsoft Global Education Exchange, Ninatarajia kujifunza mengi. Asante Microsoft.

Baada ya picha yake Owura Kwadwo kusambazwa sana kwenye mitandao ya kijamii ya Facebook na Twitter, kampuni ya Microsoft ilivutiwa na mwalimu huyo na kumpatia msaada wa vifaa vya kumsaidia katika kazi yake.