Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kim Jong-un aishukuru Korea Kusini kwa makaribisho mema
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un ameisifu Korea Kusini kwa jitihada zake nzuri za kuukaribisha ujumbe kutoka Kaskazini wakati wa mashindano ya olimpiki ya msimu wa baridi.
Matamshi yake yanakuja huku ujumbe, ulioongozwa na dada yake Kim Yo-jong uliporejea nyumbani kutoka Pyeongchang.
Shirika la habari la serikali KCNA lilisema kuwa Bw Kim aliishukuru Korea Kusini kwa kuupigia debe uwepo wake katika mbio hizo.
Kuhudhhuria kwa Korea Kaskazini kumekuwa kwa mchango mkubwa kwa uhusiani kati ya nchi hizo.
Lakini kumekuwa pia na wasi wasi kuwa hiyo imeruhusu Korea Kaskazini kufanikiwa katika propaganda zake.
Bi Kim na mkuu wa nchi asiye na madarakani Kim Yong-nam waliakuwa miongoni mwa maafisa wakuu waliokuwa kwenye ujumbe wa Korea Kaskazini kuzuru Korea Kusini tangu vita vya Korea Kaskazini miaka ya 1950.
Sikua ya Jumamosi Kim alimualika rais wa Korea Kusini Moon Jae-in, kuzuru Pyongyang kwa mazungumzo. Ikiwa mkutano huo utafanyika utakuw wa kwanza kwa zaidi ya muongo mmoja kati ya viongozi wa Korea mbili.
Mwaliko huo unakuja hukua uhusino kati ya Korea zote ukionekana kuboreka.