Sehemu ya helikopta ya jeshi la Marekani yaanguka shuleni Japan

US CH-53E helicopter

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Sehemu ya helikopta ya jeshi la Marekani yaanguka shuleni Japan

Sehemu ya ndege ye jeshi la Marekani imeanguka kwenye shule katika kisiwa cha Okinawa nchini Japan na kuzua upya misukosuko na watu wa eneo hilo.

Sehemu hiyo ya dirisha ilianguka kwenye uwanja wa shule na kusabisha majeraha madogo kwa mwanafunnzi mmoja.

Kisiwa cha Okinawa kina kambi kuwa zaidi ya jeshi la Marekani nchini Japan.

US CH-53E helicopter

Chanzo cha picha, Hulton Archive

Maelezo ya picha, Sehemu ya helikopta ya jeshi la Marekani yaanguka shuleni Japan

Katika miaka ya hivi karibuni, ajali kadha na visa vya uhalifu vimesababisha kuwepo upinzani dhidi ya kambi hiyo ya Marekani.

Jeshi la Marekani lilithibitisha kuwa dorisha kutoka moja ya helikopta zake ilianguka kwenye uwanja wa michezo wa shule iliyo nje ya kambi ya yake ya jeshi la wanahewa.

Okinawa Governor Takeshi Onaga shows a picture of the window that fell from the helicopter

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Gavana wa Okinawa Takeshi Onaga aonyesha picha ya dirisha iliyoanguka shuleni