Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Watu 33 wafariki kwenye ajali ya treni DRC
Radio ya umoja wa mataifa nchini DRC imesema takriban watu 33 wamefariki katika ajali ya treni.
Ajali hiyo imetokea katika mji wa Buyofwe Kusini mwa jimbo la Lualaba.
Taarifa kutoka Radio Okapi zinasema treni hiyo ilianguka kisha kuwaka moto.
Gavana wa jimbo la Lualaba Richard Muyej ameiambia BBC kwamba kuna ajali iliyotokea lakini haifahamiki ni watu wangapi waliofariki.