Milipuko yawaua watu 36 kanisani nchini Misri

Milipuko yawaua watu 36 kanisani Misri

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Milipuko yawaua watu 36 kanisani Misri

Takriban watu 36 wameuawa nchini Misri kufuatia milipuko iliyolenga waumini wa kanisa la Coptic leo Jumapili.

Watu 11 waliuawa wakati mlipuko ulitoke katika kanisa la St Mark's Coptic mjini Alexandria.

Pope Tawadros II, ambaye ni mkuu wa kanisa la Coptic alikuwa amehudhuria misa katika kanisa hilo.

Takriban watu 21 wameuwa kwenye mlipuko uliotokea katika kanisa moja kaskazni mwa Misri.
Maelezo ya picha, Takriban watu 21 wameuwa kwenye mlipuko uliotokea katika kanisa moja kaskazni mwa Misri.

Watu wengine 25 walikuwa wameuawa mapema katika kanisa la St George's Coptic, mji wa Tanta umbali wa takriban kilomita 130 kusini mashariki.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari ,Pope Tawadros hakuhumia. Msaidizi wake alisema kuwa shambulizi la Alexandria liliendeshwa na mshambuliaji wa kujitoa mhanga nje ya kanisa.

Kundi la Islamic State linasema kuwa ndilo liliendesha mashambulizi hayo.

Mwezi Disemba mwaka uliopita, watu 25 waliuawa wakati bomu lilipolipuka katika kanisa la Coptic cathedral mjini Cairo wakati wa sala.

Takriban watu 13 wameuwa kwenye mlipuko uliotokea katika kanisa moja kaskazni mwa Misri.

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Takriban watu 13 wameuwa kwenye mlipuko uliotokea katika kanisa moja kaskazni mwa Misri.

Ghasia dhidi ya wakiristo wa Coptic, zimekuwa nyingi miaka ya hivi karibuni, hasa tangu mwaka 2013 wakati jeshi lilipompindua rais aliyekuwa amechaguliwa.

Baadhi ya wafuasi wa rais aliyetimuliwa Mohammed Morsi, ambaye alitoka kundi la Muslim Brotherhood, waliwalaumu wakiristo kwa kuunga mkono kupinduliwa kwake.