China yapiga marufuku ndevu na burka Xinjiang

China yapiga marufuku ndevu ndefu na burka Xinjiang

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, China yapiga marufuku ndevu ndefu na burka Xinjiang

Sheria mpya zitaanza kutekelezwa katika jimbo la magharibi mwa Uchina la Xinjiang, ambako utawala wa Beijing unaaendeleza kile wanachokisema ni kuzuia ueneaji wa itikadi kali.

Miongoni mwa hatua wanazochukua ni kupiga marufuku mavazi ya wanawake ya niqab au burka ya kuziba uso au kufuga ndevu ndefu kwa wanaume wa jamii ya waislamu wa Uighurs.

China yapiga marufuku ndevu ndefu na burka Xinjiang

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, China yapiga marufuku ndevu ndefu na burka Xinjiang

Kumekuwa na visa vya makabiliano makali ya mara kwa mara baina ya maafisa polisi na wakaazi wa jimbo hilo la Uighurs, linalotaka kuwa na mamlaka na uhuru zaidi.

Wapinzani wa sheria hizo wanasema zinalenga kukandamiza utamaduni wa jamii ya waislamu wa wa Uighurs huko Uchina.

China yapiga marufuku ndevu ndefu na burka Xinjiang
Maelezo ya picha, China yapiga marufuku ndevu ndefu na burka Xinjiang