Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Trump akumbana na wakati mgumu kupinga uhamiaji
Majaji nchini Marekani wamempa wakati mgumu Rais Donald Trump baada ya kupinga sheria mpya ya uhamiaji inayowazuia wageni kutoka baadhi ya nchi, nyingi zikiwa za Kiislam kuingia Marekani.
Zuio hilo la majaji limekuja ikiwa ni saa chache kabla ya sheria hiyo kuanza kutumika rasmi.
Hakimu katika jimbo la Hawaii akishirikiana na wanasheria wa serikali wamesema zuio hilo litawanyima haki waislam wa Marekani sambamba na wahamiaji.
Trump amesema kuwa zuio hilo la makahama ni la kushangaza na sio haki na kupanga kuipeleka kesi hiyo katika mahakama za juu zaidi.