Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Utafiti: Binaadamu walichangia upanzi wa miti ya Amazon
Utafiti mpya umebaini kwamba jamii za jadi katika maeneo ya Amazon zilichangia pakubwa katika upanzi wa miti iliyounda misitu ya sasa asilia.
Hii ni kinyume na ilivyodhaniwa kwamba jamii hizo za jadi hazikuchangia kuwepo misitu hiyo.
Utafiti unasema jamii hizo zilitumia vyakula kama vile njugu karanga, kakao na mafuta yanayopatikana kwenye misitu hiyo.
Utafiti unasema kwamba jamii hizo ziliishi ndani ya misitu hiyo na siyo pembezoni kama ilivyokua imani ya hapo awali.