Simu ya Adolf Hitler kupigwa mnada Marekani

Chanzo cha picha, AFP/Getty Images
Simu iliyokuwa ikitumiwa na Adolf Hitler wakati wa vita vikuu vya pili vya Dunia itapigwa mnada nchini Marekani mwisho mwa juma hili.
Simu hiyo nyekundu iliyo na chapa cha jina la kiongozi huyo wa Wanazi, ilipatikana katika ngome ya Hitler jijini Berlin mwaka 1945.
Wanajeshi wa Urusi walimpa mwanajeshi wa Uingereza, Brigedia Sir Ralph Rayner, kama kito cha kumbukumbu, muda mfupi baada ya Ujerumani kukubali kushindwa katika vita hivyo.

Chanzo cha picha, AFP/Getty images
Kampuni hiyo ya mnada iliyoko Maryland, ilisema kuwa shughuli za mnada zitaanza kwa bei ya Dola 100,000.








