Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ndege ya Urusi yawaua wanajeshi wa Uturuki Syria
Rais wa Urusi Vladimir Putin ameomba msamaha baada ya shambulizi la Urusi kuwaua kimakosa wanajeshi watatu wa Uturuki kaskazini mwa Syria.
Wanajeshi hao walikuwa wakiwasaidia waasi nchini Syria, wakati wa jitihada za kuuteka mji wa al-Bab kutoka kwa kundi la Islamic State.
Hii ni sehemu ya hatua kubwa inayofanywa na Uturuki kuwatimua Islamic State, mbali na mpaka wa kusini mwa Uturuki.
Urusi na Uturuki ambao wanaunga mkono pande pinzani wamekuwa wakiwapiga vita Islamic State hivi majuzi kwa mashambulizi ya ndege.