Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Al-Shabab washambulia kikosi cha AU Somalia
Kundi la wanamgambo wa kiislamu nchini Somalia la al-Shabab, limeshambulia msafara wa kikosi cha Muungano wa Afrika kilicho nchini humo.
Shambulizi hilo lilitokea karibu na mji wa Mahadaay kati kati mwa eneo la Shabelle karibu kilomita 120 kaskazini mwa mji mkuu Mogadishu.
Wenyeji waliiambia idhaa ya kisomali ya BBC, kuwa mapigano ya kutumia silaha kubwa yaliendelea kwa karibu saa moja, lakiniki hakuna ripoti za maafa.