Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wanamgambo wa serikali, wasaka IS Sirte, Libya
Wanamgambo waliowatiifu kwa serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya wanasema wanawasaka wapiganaji wa kundi la Islamic State katika mji wa Sirte.
Baada ya miezi saba ya mapigano. Majeshi ya Libya wamekuwa wakipambana kuelekea wilaya ya al-Giza al Bahriya, eneo pekee la mjini ambalo mpaka sasa linadhibitiwa na wapiganaji wa IS.
Ingawa, serikali imeyarudisha majengo yaliyochukuliwa, maeneo hayo bado hayako na usalama karibu.
Maafisa wa jeshi wamesema baadhi ya wapiganaji hao wenye msimamo mkali wametoroka baada ya kuzingirwa.
Mwaka uliopita kundi hilo la IS waliigeuza Sirte kuwa ngome yao.