Maelfu waandamana wakimtaka rais wa Korea Kusini ajiuzulu

Maandamano yaingia wiki ya sita

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Maandamano yaingia wiki ya sita

Maelfu ya watu nchini Korea Kusini wamekusanyika kwenye mji mkuu Seoul kwa wiki ya sita mfululizo wakitaka rais Park Geun-hye ajiuzulu.

Maandamano ya hivi punde yanajiri muda mfupi baada ya vyama vya upinzani kupeleka bungeni mswada wa kumuondoa madarakani Rais Park.

Mswada huo unaoungwa mkono na wabunge 170 unapigiwa kura wiki ijayo.

Rais Park Geun-hye

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Rais Park Geun-hye

Rais Park amesema kuwa ana nia ya kuondoka madarakani kufuati madai kuwa walishirikiana na rafiki wake wa karibu Choi Soon-sil, ambaye anakabiliwa na mashataka ya ufisadi.