Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mfalme akamatwa kwa kuchochea ghasia Uganda
Polisi nchini Uganda wanasema watu 50 wameuawa, katika mapambano baina ya askari wa usalama na kundi jipya lenye silaha, linalopigana kutaka kujitenga, magharibi mwa nchi.
Polisi wamemkamata mfalme wa kabila la huko, Charles Wesley Mumbere, mfalme wa Rwenzururu, ambaye wanamshutumu kwa kuchochea fujo hizo.
Amekanusha kuwa amehusika.
Polisi pia wanasema wamewakamata wapiganaji kadha walipovamia kasri ya mfalme huyo mjini Kasese, karibu na mpaka wa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo.
Eneo hilo dogo limekuwa na mvutano na serikali ya Uganda kwa muda mrefu, na linavutana piya na eneo la Mfalme wa Toro.