Hillary Clinton aenda kutembea porini

Picha ya Margot Gerster, mtoto wake na Bi Hillary Clinton

Chanzo cha picha, Facebook - Margot Gerster

Maelezo ya picha, Picha ya Margot Gerster, mtoto wake na Bi Hillary Clinton

Mwanamke mfuasi wa chama cha Democratic ambaye alivunjwa moyo na kushindwa na Bi Hillary Clinton amekutana na mtu asiyemtarajia porini, mgombea huyo mwenyewe.

Margot Gerster alienda matembezi akiwa na binti yake na mbwa katika msitu wa Chappaqua, New York.

Hakutarajia kukutana na Bi Clinton ambaye alishindwa na Donald Trump wa Reublican siku mbili awali, lakini hilo ndilo lililotokea.

Picha yake pamoja na Hillary Clinton ndiyo mara ya kwanza Bi Clinton kuonekana hadharani tangu atoe hotuba ya kukubali kushindwa Jumatano.

Bi Gerster anasema picha hiyo ilipigwa na mumewe Hillary Clinton, Bill.

Grey line

Bi Gerster, ambaye huishi White Plains, amesimulia kuhusu kisa hicho kwenye Facebook.

Ujumbe wake ulipendwa mara zaidi ya 110,000 na kusambazwa na watu 9,000 kabla yake kuufanya wa faraghani.

"Nilimkumbatia na kuzungumza naye na kumwambia kwamba moja ya nyakati ninazojivunia zaidi kama mama ni wakati ambao nilimbeba Phoebe nikaenda naye na tukampigia kura," amesema.

"Alinikumbatia na kunishukuru na tukasemezana na kisha nikamwacha aendelee na matembezi."

Facebook post by Margot Gerster shows picture of her with Hillary Clinton and says: "I've been feeling so heartbroken since yesterday's election and decided what better way to relax than take my girls hiking. So I decided to take them to one of favorite places in Chappaqua. We were the only ones there and it was so beautiful and relaxing. As we were leaving, I heard a bit of rustling coming towards me and as I stepped into the clearing there she was, Hillary Clinton and Bill with their dogs doing exactly the same thing as I was. I got to hug her and talk to her and tell her that one of my most proudest moments as a mother was taking Phoebe with me to vote for her. She hugged me and thanked me and we exchanged some sweet pleasantries and then I let them continue their walk. Now, I'm not one for signs but I think ill definitely take this one. So proud.

Chanzo cha picha, Facebook - Margot Gerster

Bi Clinton na mumewe huishi Chappaqua, wilaya ya Westchester, na ni eneo hilo ambapo Bi Clinton alipiga kura Jumanne.

Na haionekani kana kwamba hiyo ilikuwa mara ya kwanza kwa Bi Gerster kukutana na waziri huyo wa zamani wa mambo ya nje.

Alipakia mtandaoni picha yake na Bi CLinton, ambaye anasema alipigwa picha naye alipokuwa shule ya pili, wakati wa hafla ya kuchangisha pesa iliyoandaliwa na mamake.

Bi Clinton alikuwa mgeni wa heshima.