Kwa Picha: Uvuvi wa pweza Zanzibar

Chanzo cha picha, Tommy Trenchard
Mchanga mweupe wa bahari kutoka mashariki mwa pwani ya Zanzibar husifika sana kama eneo la mapumziko.
Lakini kila siku, wakati maji yanajaa na watalii wanarudi hotelini, kundi dogo la wanawake na wanaume wakiwa wamebeba fimbo na mishale wanaelekea baharini kutafuta mojawapo ya vyakula vitamu vya kisiwa hicho cha Tanzania - pweza.

Chanzo cha picha, Tommy Trenchard
Wakati maji yakikupwa mara moja mvuvi wa pweza aliye na ujuzi anaweza kunasa takriban pweza 10 wanaoishi katikati mwa mawe, matumbawe na nyasi za baharini.
Samaki hao wanaouzwa kwa bei ghali katika hoteli za kitalii na huwa na protini ya hali ya juu kwa jamii zinazoishi pwani.

Chanzo cha picha, Tommy Trenchard
Matumbawe huwa chanzo cha kujikimi maisha kwa wakaazi wa eneo hilo maana hupata samaki kama vile kaa, na pweza.

Chanzo cha picha, Aurelie Marrier d'Unienville
Pweza wengi hupatikana Tanzania magharibi mwa bahari Hindi.

Chanzo cha picha, Tommy Trenchard
Abdullah Ali, mwenye umri wa miaka 35, ajitayarisha kuodnoka na boti lake la mbao ili kuwinda pweza kutoka kijiji cha Dongwe.
Hii imekuwa kazi ya wanawake kitamaduni lakini wanaume pia sasa wamejishughulisha na kazi hiyo ya uindaji kutafuta riziki.

Chanzo cha picha, Aurelie Marrier d'Unienville
"Pweza wamenisaidia kusukuma maisha," anasema Ali, anayejipatia $2.30 kwa kila kilo ya pweza.

Chanzo cha picha, Tommy Trenchard
Kwa mujibu wa data kutoka shirika la umoja wa mataifa la chakula na kilimo FAO, uwindaji pweza umeongezeka Tanzania kutoka tani 482 mnamo 1990 hadi 1,250 mwaka 2012.

Chanzo cha picha, Tommy Trenchard
Mwamba na mandhari ya bahari yanatoa nafasi kwa pweza kujificha wakati maji yamekupwa baharini, na kufanya vigumu kuonekana kwa mtu asiye na uzoefu.

Chanzo cha picha, Tommy Trenchard
Mariam, muindaji pweza kutoka kijiji cha Bwejuu village, anazama ndani ya maji kupunguza joto baada ya kazi ya asubuhi.

Chanzo cha picha, Tommy Trenchard
Mama Juma, muindaji wa pweza, anakagua maji karibu na mwamba wa Paje katika maenoe ambayo huenda pweza wamejificha.

Chanzo cha picha, Aurelie Marrier d'Unienville
Mwanamke atafuta pweza jioni huko Bwejuu.
Jamii hutegemea samaki hao wa maji madogo kujikimu kimaisha.

Chanzo cha picha, Tommy Trenchard
Pweza wa kuchomwa ni chakula maarufu kinachouzwa katika soko la samaki usiku Stone Town.
Pweza wengi wanaovuliwa Tanzania bara husafirishwa Ulaya, lakini utalii katika kisiwa cha Zanzibar umetoa soko kubwa.












