Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wiki ya Afrika katika picha: 18-24 Novemba 2022
Uteuzi wa picha bora za wiki kutoka bara zima na kwingineko:
Mashabiki wa soka wa Cameroon wakiwa wamevalia vizuri wakati Indomitable Lions ikimenyana na Uswizi siku ya Alhamisi kwenye Kombe la Dunia nchini Qatar, timu yao ingawa imefungwa bao 1-0...
Tunisia yaizima Denmark na kupata sare ya 0-0 huku familia hii ya mashabiki ikishabikia siku ya Jumanne...
Shindano hilo litaanza Jumapili na watoto hawa katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, watafurahia tukio hilo kwenye maonyesho ya umma.
Siku ya Jumatatu, mkaazi aliyekata tamaa katika kitongoji kimoja katika mji wa Cape Town nchini Afrika Kusini anajaribu kuzima moto unaoharibu nyumba yake.
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amekaribishwa nchini Vietnam anaposafiri kwa ndege kuelekea Hanoi siku ya Alhamisi katika safari ya kuboresha uhusiano na nchi hiyo.
Mpiga picha akimnasa mhitimu mpya ambaye alikuja kuwa mwanajeshi wa Sudan Kusini kwenye sherehe mjini Malakal siku ya Jumatatu...
Waajiri wapya wanakaribishwa katika jeshi la polisi kwa wakati mmoja.
Mfalme Charles III amchekesha Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa siku ya Jumanne wakati anaandaa karamu ya kitaifa kwa heshima yake - ya kwanza ya utawala wake.
Siku hiyo hiyo katika mji mkuu wa Angola, Luanda, mashabiki wa mwanamuziki kuduro Nagrelha wanafanya maandamano kwa heshima yake kufuatia kifo chake cha ghafla kutokana na saratani ya mapafu.
Watu huko Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wanafanya mazoezi ya yoga siku ya Jumapili.
Muda mfupi kabla ya Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa kuwasili katika bunge jipya la nchi hiyo siku ya Jumatano mwanajeshi akirekebisha sare ya mwenzao ili kuhakikisha kila kitu kiko sawa.
Picha zina hakimiliki.