Hivi ndivyo almasi hii kutoka Afrika ilipoishia kumilikiwa na familia ya Malkia Elizabeth

ggg

Chanzo cha picha, Getty Images

Almasi kubwa zaidi katika taji la kifalme lenye Vito vya thamani nchini Uingereza inaweza kuwa vipande vya kale vya sakafu ya bahari, ambayo ilibebwa na mkondo wa maji hadi chini dunia yetu na kisha kurudi juu tena.

Kifurushi kilifika kwenye sanduku la kadibodi la kawaida. Ilielekezwa katika anwani ya S Neumann & Co - wakala wa mauzo ya madini katikati mwa London na ilikuwa na uzito wa zaidi ya pauni moja (karibu 500g). Lakini hii haikuwa mizigo ya kawaida.

Ilikuwa Aprili 1905, na miezi mitatu nyuma, meneja katika Mgodi wa Premier nchini Afrika Kusini alikuwa akikamilisha ukaguzi wa kawaida wa futi 18 (5.4m) chini ya ardhi wakati akitazama mwanga ulioakisiwa kwenye ukuta mbovu juu yake.

Alidhani ni kipande kikubwa cha glasi kilichochongwa na wenzake kama mzaha. alitoa kisu chake cha mfukoni na baada ya kuchimba… kisu kikachomoa mara moja.

Hatimaye mwamba huo uliondolewa kwa mafanikio, na kuonesha kuwa ni almasi halisi jiwe kubwa la karati 3,106.75, ikiwa karibu na ukubwa wa ngumi. Haikuwa kubwa tu, lakini ung'aavu usio wa kawaida.

Cullinan, kama ilivyojulikana, ni almasi kubwa zaidi kuwahi kupatikana. Mara tu ilipong'arishwa na kung'olewa katika mawe kadhaa yanayoweza kudhibitiwa, kioo kikubwa zaidi ambacho kilitoa mng'ao wa nyota katika mfumo wa nyota wa mbali.

Kwa hiyo, jiwe hili - Cullinan I - wakati mwingine hujulikana kama Nyota Kuu ya Afrika.

Karibu miaka 120 baadaye, almasi hiyo kubwa zaidi haijasahaulika. Wakati wa msafara wa mazishi wa marehemu Malkia Elizabeth II, vizazi kadhaa vya Cullinan viliwekwa kwenye jeneza la Malkia, na zilitembea pamoja naye na kuondolewa tu jeneza lilipokuwa likishushwa kwenye chumba cha kifalme kwa mazishi.

Hiyo ni kwa sababu leo hii jiwe hilo kubwa la thamani ​ni sehemu ya Vito vilivyopo katika Taji hilo la kifalme, ambavyo kwa kawaida huwekwa katika jumba la makumbusho la taji la vito (London Tower) na kuletwa nje kwa matukio ya serikali.

Cullinan I sasa inakaa katika Fimbo ya Mfalme wa Uingereza, wakati ndugu yake wa pili, Cullinan II, imepachikwa katika Taji la kifalame lenye vito vya thamani

Hata hivyo, kabla almasi chafu haijaweza kubadilishwa na kuchukua nafasi yake katika historia, ilihitaji kuuzwa na London ilichaguliwa kama sehemu nzuri zaidi ya kufanya hili. Hili lilileta tatizo: unawezaje kusafirisha jiwe la thamani kama hilo maili 7,926 (km 12,755), bila kuibiwa?

ggg

Chanzo cha picha, Getty Images

Hauhitaji Whatsapp
BBC Swahili sasa kwenye WhatsApp

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Bonyeza hapa kujiunga

Mwisho wa Whatsapp

Mwishowe, jiwe hilo la thamani lilitumwa kutoka Johannesburg na posta ya kawaida, kwa gharama ya shilingi tatu tu au kama Senti 75 za Marekani wakati huo (karibu £11.79 au $13.79 leo).

Wakati huo huo, mfano wa almasi ambayo haikuwa halisi ilifanya safari ndefu kwenda London kwa boti ya mvuke iliwekwa waziwazi sehemu salama ya nahodha na ililindwa na polisi wapelelezi kama mapambo tu.

Kwa kushangaza, zote zilifanikiwa kufika. Baada ya miaka mingi ya kushindwa kuuzwa, almasi halisi iliyosafirishwa kwa posta ya kawaida, wakati huu - ilinunuliwa na serikali ya Transvaal kwa £150,000 (£20m au US$22.5m leo) na kupewa zawadi King Edward VII.

Lakini ingawa zinajulikana kote ulimwenguni kwa ukubwa na angavu, sifa hizi sio ajali. Cullinan ilikuwa almasi ya "Clippir" - jamii ya madini ya kipekee ambayo ni makubwa zaidi na ya kung'aa zaidi kuwahi kupatikana. Na kuna zaidi ya hivyo kuliko inavyoonekana.

Pamoja na uzuri wao wote, almasi ni vipande vya ndani zaidi katika Dunia - vitu visivyo vya kwaida vya kijiolojia vinavyovutia ambavyo vimefichwa kama vito tu.

Miamba ya ajabu kutoka katika ulimwengu mwingine - eneo la ajabu lisiloweza kueleweka, lililozungukwa na miamba ya kijani kibichi na madini ambayo hayapatikani, chini kabisa ya uso wa Dunia.

Wanasayansi kote ulimwenguni wamekuwa wakitafiti kwa miongo kadhaa ili kufichua siri za eneo hilo na cha kushangaza, ni almasi ambazo tunathamini zaidi ambazo zina hadithi zisizo za kawaida za kusimulia. Kwa kweli, mawe makubwa kama Cullinan yanabadilisha uelewa wetu wa ndani ya sayari yetu.

Fursa isiyo ya kawaida

Akiwa ameketi mbele ya darubini katika Taasisi ya Gemological ya Marekani (GIA) mnamo 2020, Evan Smith alinyoosha glavu za mpira juu ya vidole vyake kwa uangalifu, na kuchungulia kwenye lenzi za kifaa. Chini yake kulikuwa na almasi yenye karati 124 za uzuri wa ajabu.

Kufikia hatua hii, Smith alikuwa tayari amepitia karibu viwango vya usalama vya kijeshi - uchunguzi wa Isis scans na ukaguzi wa utambulisho, ikifuatiwa na tabaka baada ya tabaka la milango iliyofungwa, lifti salama na korido zenye vikwazo vya ajabu. Wakati akifanya kazi, kamera za video zilionesha vizuri muonekano wa chumba hicho kuangalia walinzi waangalifu.

ggg

Chanzo cha picha, Alamy

Maelezo ya picha, Taji lenye Madini la Kifalme lina almasi mbili zinazoshukiwa kuwa zenye kina kirefu, Cullinan II (pia inajulikana kama Nyota ya Pili ya Afrika) na Koh-i-Noor maarufu

Smith mwanasayansi mkuu wa utafiti katika GIA - alikuwa akichunguza almasi kwa ujumla, jinsi kioo cha almasi kinavyoundwa na chini ya hali gani. Lakini kufanya kazi ya almasi za thamani ya juu ni biashara ngumu

Maya Kopylova, profesa wa uchunguzi wa madini katika Chuo Kikuu cha British Columbia, anasema kupata sampuli za almasi yoyote ni ngumu, na almasi nyingi anazofanya nazo kazi zingeweza kutupwa.

"Watafiti wanapaswa kuwa na uhusiano mzuri na makampuni na kamwe hawatakupa sampuli muhimu," anasema. "Kwa hivyo, hawataweza kutupatia almasi ambazo zina ukubwa wa 6mm (inchi 0.2) au kubwa zaidi."

Alichogundua Smith kilikuwa cha mapinduzi. Takriban robo tatu ya almasi ya Clippir ilikuwa na mifuko midogo midogo, au "mipako" ya chuma ambayo iliepuka kutu sio kitu ambacho ungepata katika zile za kawaida zingine zilizobaki zilikuwa na aina ya garnet ambayo safu msingi ya juu huyeyuka.

Kwa utafiti wake wa 2020 - pamoja na Wuyi Wang, ambaye ni makamu wa rais wa utafiti na maendeleo huko GIA - Smith alichambua almasi ya karati 124 na kugundua kuwa iliundwa kwenye mwisho wa kina wa safu inayowezekana - angalau 660km (maili 410) chini ya uso wa dunia.

Snake

Chanzo cha picha, Alamy

Maelezo ya picha, Baadhi ya kaboni katika almasi yenye kina kirefu zaidi inaweza kuwa kutoka kwa viumbe vya kale vya baharini, ambavyo vilizikwa kwenye mabamba ya bahari ambayo baadaye yalipeperushwa hadi juu

Kutoka kwenye kina

"Kwa mtazamo wa kijiolojia, almasi [kwa ujumla] ni madini ya ajabu sana," tunawekeza makumi ya mamilioni kila mwaka katika harakati zetu za kuzitafuta - zaidi ya bajeti ya mradi wowote wa utafiti.

Na ingawa juhudi hizi zimesababisha uharibifu mkubwa, kuanzia vita na ukoloni hadi kugeuza mito na kuinua makazi adimu, kama si shauku yetu kwa madini haya yanaong'aa "tusingewahi kuzipata na kuzitafiti,” anasema Smith.

Hata almasi za kawaida zaidi ni za kipekee kati ya miamba, hutengenezwa katika kina cha ndani zaidi kuliko nyingine yoyote - hakuna kitu kingine chochote kwenye uso wa Dunia ambacho kimeibuka kutoka chini ya dunia yetu.

"Hakuna nyenzo nyingine kwenye uso inayotoka kwa kina cha kilomita 600 [maili 373], sivyo," anasema Kopylova. Magma ambayo hutufikia hutoka karibu kilomita 400 [maili 249] chini, lakini tofauti na almasi, ambayo hufika usoni bila kubadilika, hii ni mwamba ulioyeyuka.

"Na hiyo inaongeza kiwango kingine cha kutokuwa na uhakika wa kile kilikuwa nyenzo asili kabla ya kuathiriwa na kuyeyuka," anaongeza Kopylova.

Baada ya almasi kuundwa, inachukua mlolongo wa michakato isiyowezekana ili kuileta juu ya uso. Kwanza, harakati za asili za miamba yenye joto kali huileta karibu na uso kwa mamia ya mamilioni ya miaka, ikiwezekana kama sehemu ya "maporomoko" kubwa ambazo zinaweza kunyoosha maelfu ya kilomita kutoka ukingo wa msingi hadi eneo la juu.

Snake

Chanzo cha picha, Getty Images

Lakini kwa miongo kadhaa, almasi nyingi zilizopatikana kutoka ndani zaidi ya Dunia zilikuwa ndogo na sio muhimu sana. Kutafiti almasi kubwa, ghali, daima imekuwa gumu hakuna mtu ambaye alikuwa ameangalia ikiwa zinaweza pia kutoshea katika kitengo hiki.

"Hatukuwahi kuzifikiria kama kitu ambacho kinaweza kuwa ubora kwa vito - kwamba tutawahi kuvaa almasi za kina kirefu au, kuziweka kwenye taji au fimbo au kitu kama hicho," anasema Smith.

Kiini cha mwisho katika utafiti wa Smith wa 2020 kilikuwa madini ambayo hayakupatikana ambayo yalionekana kwa mara ya kwanza miaka sita iliyopita- ilipatikana katika mabaki magumu yenye umri wa miaka bilioni 4.5 ambayo yalianguka kwenye Dunia mwaka 1879.

Inafikiriwa kuwa mwamba wa zamani wa nje ya ardhi hapo zamani ulikuwa sehemu ya kitu kikubwa zaidi cha angani, asteroid, na kuvunjika wakati wa athari mbaya. Wakati wa mchakato, ilipata shinikizo la juu sana, sawa na zile zinazopatikana ndani ya Dunia.

Meteorite ya Tenham, kama inavyojulikana, ilivunjika ilipokuwa ikianguka, na kutawanya vipande huko Queensland, Australia ambavyo vingi vilikusanywa na hatimaye kupewa zawadi kwa Makumbusho ya Uingereza huko London na mjane wa mwanajiolojia.

Miaka 143 mbele, vipande hivyo vimechunguzwa sana, hasa kwa yale ambayo wanaweza kutuambia kuhusu mambo ya ndani ya sayari yetu.

Na mnamo 2014, wanasayansi waligundua bridgmanite madini makubwa zaidi ya ndani ya moja ya miamba hii.

Kwa kushangaza, vito vya carat 124, Smith alitafiti vilivyomo ndani ya madini haya, licha ya hali yake ya kuharibika hata ndani ya almasi

Lakini kwa nini haya yote yanafanya almasi zenye kina kirefu kuwa tofauti sana? Na wanaweza kutuambia nini kuhusu ulimwengu uliofichwa ambao wameumbwa ndani yake?

Snake

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Leo almasi nyingi za kina kirefu hutoka kwenye mgodi wa Cullinan nchini Afrika Kusini, na mgodi wa Letsseng katika nchi jirani ya Lesotho

Kaboni ya kale

Kulingana na Smith, sifa zisizo za kawaida za almasi kubwa na yenye thamani zaidi ulimwenguni zote zinatokana na jinsi zinavyoundwa.

Hata asili ya almasi ya kawaida bado haieleweki, lakini inafikiriwa kuanza maisha kama majimaji - kuna uwezekano mkubwa kwamba maji ya kale ya bahari yamenasa chini ya ardhi pamoja na mabamba ya bahari yanayozama.

Kwa namna fulani, labda kutokana na mabadiliko ya ghafla ya halijoto au shinikizo, maji haya yenye madini mengi huishia kukataa kaboni inayoyeyushwa ndani yake, ambayo hutoka nje na chini ya shinikizo kubwa chini ya ganda la Dunia, kaboni hubadilika kuwa almasi.

Lakini almasi zenye kina kirefu kama Cullinan ni tofauti. Badala ya kuanzia ndani ya maji, zenyewe huanza maisha kama kaboni iliyoyeyushwa ndani ya chuma chenye maji, chini kabisa katika mambo ya ndani ya sayari.

"Ni kama chuma iliyoyeyuka na salfa na kaboni iliyoyeyushwa humo," anasema Smith. "Kwa hivyo ni aina tofauti kabisa ya maji, lakini bado ni maji ya kaboni. Inapitia mabadiliko yoyote ya kemikali au joto, na hiyo inasababisha kaboni kung'aa." Katika kesi hii, maji ya awali yana nitrojeni kidogo, kwa hivyo huishia na kitu kidogo sana - na kwa hivyo ni wazi zaidi.

Kwa kifupi, almasi za Clippir sio za kawaida tu ambazo zimekua kwa viwango vya kushangaza ni tofauti kimsingi.

Kwa kweli, ukubwa wao usio na usawa na angavu ni matokeo ya moja kwa moja ya njia isiyo ya kawaida innayounda. Na tangu kugunduliwa kwao, almasi zenye kina kirefu zaidi zimefichua baadhi ya siri zinazolindwa kwa karibu zaidi za sayari yetu.