Papa Francis akiri kukosa uvumilivu usiku wa mwaka mpya

Papa Francis
Muda wa kusoma: Dakika 1

Papa Francis ameomba radhi kwa kitendo chake cha kumchapa kibao, mmoja wa waumini kwenye kanisa la St Peter's Square huko Rome.

Papa alikuwa akisalimiana na watoto na mahujaji na wakati akigeuka mwanamke mmoja aliyekuwa kwenye umati wa watu waliokuwa karibu aliuvuta mkono wa Papa kwa nguvu karibu amuangushe.

Hali iliyomfanya Papa kugeuka na kumpiga makofi mawili mkononi mwanamke huyo kwa hasira.

Papa akiwa anavutwa na muumini
Maelezo ya picha, Papa akiwa anavutwa na muumini

Badaye Papa alikiri kwamba alishindwa kujizuia na yeye pia huwa anakosea kama binadamu wengine.

Hivyo anaomba radhi kwa kitendo hicho kwa muumini huyo na kila mtu.

Kitendo cha Papa cha kumzaba makofi ya mkononi mwanamke huyo, kimezua mjadala kwenye mitandao ya kijamii, hasa Twitter, wengi wakimuunga mkono Papa.

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe

Awali wakati wa hotuba yake ya mwaka mpya, Papa alikemea unyanyasaji dhidi ya wanawake.