Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mafuriko yasababisha maafa makubwa Ugiriki
Vikosi vya uokoaji nchini Ugiriki vinasema takriban watu kumi na nne wanahofiwa kufariki baada ya mafuriko makubwa kutokea karibia na mji mkuu Athens.
Wanasema wanatarajia kuopoa miili ya watu wengi zaidi.
Maji yamezingira kila kona ya mji kutokana na mvua kali.
Nyumba za makaazizile za biashara pamoja na barabara zimeharibiwa vibaya.
Meya wa mji wa Nea Peramos uliopo Magharibi mwa Athens amesema juhudi za haraka za uokoaji zinahitajika.
Mafuriko hayo yanatajwa kuwa mabaya zaidi kwa kipindi cha miaka ishirini iliyopita.