Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wafilipino wakataa aliyekuwa rais kuzikwa katika makaburi ya mashujaa
Zaidi ya wafilipino 1000 wameandamana mjini Manila dhidi ya mpango wa kuuzika mwili wa Rais wa zamani aliyefedheheshwa , Ferdinand Marcos, kwenye eneo la mashujaa wa taifa hilo.
Waandamanaji hao walihimili mvua kubwa iliokuwa ikinyesha, na kumuomba rais wa sasa , Rodrigo Duterte, kufuta mpango huo.
Mwaandamanaji mmoja, seneta Risa Hontiveros, amemtaja rais Duterte kuwa adui wa mashujaa wa Ufilipino.
Rais huyo wa awali anatuhumiwa kuhusika katika ufisadi , na ukiukaji wa haki za binaadamu.
Serikali yake ilipinduliwa mwaka wa 1986, na aliaga dunia akiwa uhamishoni miaka mitatu baadaye.