Unai Emery: Kocha wa Arsenal afutwa kazi

Mkufunzi wa Arsenal Unai Emery amefutwa kazi baada ya kuongoza timu hiyo kwa kipindi cha miezi 18.

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Mkufunzi wa Arsenal Unai Emery amefutwa kazi baada ya kuongoza timu hiyo kwa kipindi cha miezi 18.
Muda wa kusoma: Dakika 2

Mkufunzi wa Arsenal Unai Emery amefutwa kazi baada ya kuongoza timu hiyo kwa kipindi cha miezi 18.

Raia huyo wa Uhispania , ambaye awali alikuwa mkufunzi wa Paris St-Germain katika ligi ya Ufaransa na kushinda mataji matatu ya Yuropa akiwa na Sevilla, aliteuliwa kuwa mkufunzi wa Arsenal mwezi Mei 2018, akimrithi Arsene Wenger.

Mahala pake patachukuliwa kwa muda mfupi na aliyekuwa kiungo wa kati wa Arsenal Freddie Ljungberg.

Arsenal inasema kwamba uamuzi huo ulichukuliwa baada ya matokeo ya timu hiyo kushindwa kufikia kiwango kilichohitajika.

Arsenal haijashinda katika mechi saba na ilipoteza 2-1 nyumbani dhidi ya klabu ya Ujerumani Eitracht Frankfurt katika ligi ya Yuropa siku ya Alhamisi.

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe

Arsenal ilianza msimu huu wakirekodi misururu ya ushindi dhidi ya Newcastle na Burnley, lakini ushindi huo ulimalizwa baada ya kulazwa na Liverpool, kabla ya kurekodi sare mbili dhidi ya wapinzani wao wa London Tottenham na Watford.

Ushindi wao wa mwisho katika ligi ya Uingereza ulikuwa dhidi ya Bournemouth.

Freddie Ljunberg wa pili kushoto ndiye naibu wa Emery katika klabu hiyo

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Freddie Ljunberg wa pili kushoto ndiye naibu wa Emery katika klabu hiyo

Siku ya Jumamosi, walitoka sare ya 2-2 ikiwa ni ya sita msimu huu nyumbani dhidi ya Southampton, huku Alexander Lacazette akifunga goli la kusawazisha katika muda wa majeraha.

Emery ni mkufunzi wa tatu kufutwa kazi katika ligi ya England msimu huu baada ya Javi Gracia na Mauricio Pochettino.

Ushindi wa mwisho wa Arsenal ulijiri dhidi ya Vitoria Guimaraes katika ligi ya Yuropa tarehe 24 mwezi Oktoba , ambapo walihitaji mipira miwili ya adhabu kupata ushindi wa magoli 3-2.

Ljungberg ameanza kuiongoza katika mazoezi timu hiyo na taarifa ya Arsenal ilisema: Tuna matumaini na Freddie Ljunberg kutuogoza. Usakaji wa kocha mpya unaendelea na tutatoa tangazo tutakapokamilisha mpango huo.

Siku ya Jumatano , BBC Sport iliripoti kwamba Arsenal inamuona Mkufunzi wa Wolves Nuno Espirito Santo kama mrithi wa Emery.

Majina mengine yanayohusishwa na tangazo hilo ni pamoja na mkufunzi wa zamani wa Tottenham, Pochettino naibu kocha wa Manchester City Mikel Arteta na mkufunzi wa zamani wa Juventus Massimiliano Alegri na Mkufunzi wa Bournemouth Eddie Howe.

Walianza msimu huu baada ya kugharamika zaidi ya £130m walipomsaini winga Nicolas Pepe, beki wa katikati David Luiz, Beki wa kushoto Kieran Tierney, mshambuliaji Gabriel Martinelli na beki William Saliba, ambaye atajiunga msimu ujao.

Pia klabu hiyo ilimununua kwa mkopo kiungo wa kati Dani Ceballos kutoka Real Madrid.