Hawa ndio wachezaji ghali zaidi kwaliouzwa Januari

Dirisha la usajili kwa mwezi Januari 2019 linakaribia ukingoni, na litafungwa saa sita ya usiku kwa saa za Uingereza.

Kwa kawaida dirisha hili huwa ni la usajili wa kawaida na wachezaji kutolewa mikopo. Hata hivyo, kuna nyakati usajili wa pesa nyingi pia hufanyika, na wachezaji hawa ndio wanaoshiilia rekodi ya kununuliwa kwa pesa nyingi mpaka sasa katika Ligi ya Premia:

2018: Philippe Coutinho alijiunga na Barcelona kutoka Liverpool kwa pauni milioni 142

2018: Virgil van Dijk ajiunga na Liverpool kutoka Southampton kwa pauni milioni 75

2017: Oscar ajiunga Shanghai SIPG kutoka Chelsea kwa pauni milioni 60

2018: Diego Costa ajiunga na Atletico Madrid kutoka Chelsea kwa pauni milioni 59

2019: Christian Pulisic ajiunga na Chelsea kutoka Borussia Dortmund kwa pauni 58

2018: Aymeric Laporte ajiunga na Man City kutoka Athletic Bilbao kwa pauni milioni 57

2018: Pierre-Emerick Aubameyang ajiunga na Arsenal kutoka Borussia Dortmund kwa pauni milioni 56

2011: Fernando Torres ajiunga na Chelsea kutoka Liverpool kwa pauni milioni 50

2014: Juan Mata ajiunga na Man United kutoka Chelsea kwa pauni milioni 37

2011: Andy Carroll ajiunga na Liverpool kutoka Newcastle kwa pauni milioni 35