Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mourinho arushiwa maji na maziwa kufuatia kushindwa kwa Man U
Maneja wa Manchester United Jose Mourinho amerushiwa maji na maziwa kufuati kushindwa na Manchester City huko Old Trafford.
United walikasirika kutokana na kile walichokiona kuwa kusherehekea kupindukia kwa City kufuati ushindi wa Jumapili wa bao 2-1 ambalo lilifungua mwaka wa pointi 11 kileleni.
Wachezaji wa City walisherehekea na mashabiki wao baada ya kipenga cha mwisho na maafisa wengine wakajaribu kumshawishi meneja Pep Guardiola kujiunga nao lakini akakataa.
Baada ya wachazaji kuondoka uwanjani inaeleweka kuwa Mourinho alilalamika akiwa ndani ya chumba cha kubadilishia nguo kabla ya kurudi kwa mahojiano.
Upande wa City ulijibu huku kipa wa Brazil Ederson akijibizana na Mourinho kwa lugha ya kireno.