"Unaweza kuja Kyiv": Zelensky amjibu Putin kuhusu pendekezo la lake la kufanya mazungumzo Moscow

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, katika mahojiano na ABC News, amekataa tena pendekezo la Rais wa Urusi Vladimir Putin kwenda Moscow kwa mazungumzo ya amani.

Muhtasari

Moja kwa moja

Abdalla Seif Dzungu

  1. Wanakijiji wa Sudan wanachimba kwa mikono ili kuwafikia wahanga wa maporomoko ya ardhi

    .

    Chanzo cha picha, Sudan Liberation Movement/Army

    Maelezo ya picha, Picha hii inadaiwa kuonyesha karibu makaburi 40

    Wanakijiji katika eneo la mbali la jimbo la Darfur magharibi mwa Sudan wanajaribu kuwafikia waathiriwa waliozikwa na udongo kwa mikono baada ya maporomoko ya Jumapili, shirika la misaada la Save the Children linasema.

    "Watu wanachimba kwa mikono kuokoa miili ya jamaa zao kwa vile hakuna zana au mashine", Francesco Lanino, naibu mkurugenzi wa shirika la mipango na uendeshaji wa Sudan alisema.

    Haijulikani ni watu wangapi walikufa - takwimu kutoka kwa wizara ya afya ya kitaifa inasema kuwa ni miili miwili pekee iliyopatikana, lakini kundi lenye silaha linalosimamia eneo hilo linatoa idadi ya watu kuwa 1,000.

    Shirika la Save the Children limesema takriban miili 373 imepatikana, kulingana na mkuu wa Mamlaka ya Kiraia.

  2. Trumps anasema ndege za Venezuela zitadunguliwa iwapo zitahatarisha meli za Marekani

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Rais Donald Trump ameonya kwamba, iwapo ndege za Venezuela zitaruka juu ya meli za wanamaji za Marekani na "kutuweka katika hali ya hatari, zitadunguliwa".

    Onyo lake linakuja baada ya Venezuela kurusha ndege za kijeshi karibu na meli ya Marekani kutoka Amerika Kusini kwa mara ya pili ndani ya siku mbili, maafisa wa Marekani waliambia mshirika wa BBC wa Marekani CBS News.

    Ripoti hizo zinafuatia shambulizi la Marekani dhidi ya kile maafisa wa Trump walisema ni "meli ya kubeba dawa za kulevya kutoka Venezuela" inayoendeshwa na genge, na kuua watu 11.

    Rais Nicolás Maduro amesema madai ya Marekani kuhusu Venezuela si ya kweli na kwamba tofauti kati ya nchi hizo hazihalalishi "mgogoro wa kijeshi".

    "Venezuela daima imekuwa tayari kuzungumza, kushiriki katika mazungumzo, lakini tunadai heshima," aliongeza.

    Alipoulizwa na waandishi wa habari katika Ofisi ya Oval siku ya Ijumaa nini kitatokea ikiwa ndege za Venezuela zitaruka juu ya meli za Marekani tena, Trump alisema Venezuela itakuwa "matatizo".

    Trump alimwambia jenerali wake, aliyesimama kando yake, kwamba anaweza kufanya chochote anachotaka ikiwa hali itazidi.

    Tangu arejee ofisini mwezi Januari, Trump amekuwa akizidisha juhudi zake za kupambana na ulanguzi wa dawa za kulevya huko Amerika Kusini.

    Maduro ameishutumu Marekani kwa kutaka "mabadiliko ya serikali kupitia vitisho vya kijeshi".

  3. Utawala wa Trump unasema mhamiaji Abrego anaweza kufukuzwa Eswatini

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Abrego Garcia

    Utawala wa Trump siku ya Ijumaa ulifichua mpango wa kumpeleka Kilmar Abrego katika taifa dogo la Afrika la Eswatini.

    Abrego ambaye kukamatwa kwake na jitihada za kubaki Marekani ndio zimekuwa kitovu cha mvutano katika msako wa uhamiaji.

    Afisa wa Wizara ya Usalama wa Ndani ya Marekani alisema kupitia barua pepe kwa mawakili wa Abrego kwamba Eswatini, zamani ikijulikana kama Swaziland, imechukua nafasi ya Uganda kama nchi iliyoteuliwa kwa ajili ya kumpeleka.

    Afisa huyo alisema mabadiliko hayo yalifanyika kwa sababu Abrego ameeleza kuwa anaogopa mateso au kuteswa nchini Uganda.

    “Madai hayo ya hofu ni magumu kuchukuliwa kwa umakini, hasa ikizingatiwa kwamba umedai (kupitia mawakili wako) kuwa unaogopa mateso au kuteswa katika angalau nchi 22 tofauti …

    Hata hivyo, tunakujulisha kwamba nchi yako mpya ya kufukuzwa ni Eswatini, Afrika,” afisa huyo alisema kwenye barua pepe.

    Abrego, asili yake akiwa El Salvador na ambaye kwa sasa anashikiliwa katika kituo cha kizuizi cha uhamiaji huko Virginia, hana uhusiano wowote na Eswatini, taifa lisilo na pwani linalopakana na Afrika Kusini.

    Msukumo wa utawala wa Trump wa kutaka kumpeleka Abrego, mwenye umri wa miaka 30, Eswatini ni sura ya hivi karibuni katika sakata lililoanza Machi, wakati mamlaka za Marekani zilipomshutumu kwa kuwa mwanachama wa genge na kumpeleka kwenye gereza la El Salvador licha ya agizo la jaji wa Marekani lililokataza kufukuzwa kwake nchini mwake.

    Abrego alirudishwa Juni ili kukabiliana na mashtaka ya jinai ya kusafirisha wahamiaji waliokuwa wakiishi Marekani kinyume cha sheria. Amejitetea kuwa hana hatia na mawakili wake wamemshutumu utawala huo kwa mashtaka ya kulipiza kisasi.

  4. Misri inasema kuelezea kuhama kwa Wapalestina kama hiari ni 'upuuzi'

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri Badr Abdelatty

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Badr Abdelatty, alisema Jumamosi kwamba kuelezea uhamisho wa Wapalestina kama wa hiari ni “upuuzi.”

    Awali, Israel iliwataka wakazi wa Jiji la Gaza kuhamia kusini, huku vikosi vyake vikisonga zaidi ndani ya eneo kubwa zaidi la mijini la Ukanda huo.

    Vikosi vya Israel vimekuwa vikitekeleza mashambulizi katika vitongoji vya jiji la kaskazini kwa wiki kadhaa, baada ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, kuagiza jeshi kuchukua eneo hilo.

    Netanyahu anasema Jiji la Gaza ni ngome ya Hamas na kulidhibiti ni muhimu ili kuwashinda wapiganaji wa Kiislamu wa Kipalestina, ambao shambulio lao dhidi ya Israel mnamo Oktoba 2023 liliuchochea vita.

    Vita vya Gaza vimezidi kuiacha Israel ikiwa pweke kidiplomasia, huku baadhi ya washirika wake wa karibu wakilaani operesheni hiyo iliyoharibu vibaya eneo hilo dogo la Gaza.

  5. Jeshi la Israel lawataka wakaazi wa mji wa Gaza kuondoka

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Wapalestina waliofurushwa na makazi ya jeshi la Israel katika shule ya UNRWA, huko Khan Younis, kusini mwa Ukanda wa Gaza, Agosti 19, 2025.

    TEL AVIV, Septemba 6 (Reuters) - Jeshi la Israeli Jumamosi lilisema Wapalestina katika Jiji la Gaza, eneo kubwa zaidi la mijini, wanapaswa kuondoka kuelekea kusini, na kuonya kwamba jeshi lilikuwa likifanya kazi katika jiji lote.

    Majeshi ya Israel yamekuwa yakifanya mashambulizi katika viunga vya mji huo wa kaskazini kwa wiki kadhaa baada ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuamuru jeshi kuuteka.

    Netanyahu anasema Mji wa Gaza ni ngome ya Hamas na kuuteka ni muhimu ili kuwashinda wapiganaji wa Kiislamu wa Palestina, ambao mashambulizi yao ya Oktoba 2023 dhidi ya Israel yalizua vita.

    Shambulio hilo linatishia kuwafurusha mamia kwa maelfu ya Wapalestina wanaojihifadhi huko kutokana na mapigano ya takriban miaka miwili. Kabla ya vita, karibu watu milioni moja, karibu nusu ya wakazi wa Gaza, waliishi katika mji huo.

    Msemaji wa jeshi la Israel Avichay Adraee aliandika kwenye X kwamba wakaazi wanapaswa kuondoka katika mji huo kuelekea eneo lililotengwa la pwani la Khan Younis kusini mwa Gaza, na kuwahakikishia wale wanaokimbia kwamba wataweza kupata chakula, matibabu na makazi huko.

    Siku ya Alhamisi, jeshi lilisema lilikuwa na udhibiti wa karibu nusu ya mji. Inasema inadhibiti takriban 75% ya Gaza yote.

  6. Morocco ni timu ya kwanza ya Afrika kufuzu katika kombe la Dunia 2026

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Morocco imekuwa nchi ya kwanza kufuzu katika Kombe la Dunia la Fifa la 2026 baada ya kuicharaza Niger 5-0 .

    Simba hao wa Atlas, ambao waliweka historia ya kutinga nusu fainali Qatar 2022, ilijua pointi tatu zingetosha kusonga mbele kutoka Kundi E ikiwa na michezo miwili tu baada ya Tanzania kupata sare ya 1-1 dhidi ya Congo-Brazzaville mapema Ijumaa.

    Mchezaji wa Niger, Abdoul-Latif Goumey alitolewa nje kwa kosa la pili dakika ya 26 na Ismael Saibari alifunga krosi ya Youssef Belammari na kufunga bao dakika tatu baadaye.

    Saibari alifunga bao la pili kabla ya kipindi cha mapumziko alipoingiza mpira wa chini kutoka kwa Achraf Hakimi na Ayoub El Kaabi akafunga bao la tatu mapema kipindi cha pili kutoka kwa Belammari.

    Mshambulizi wa zamani wa Rangers, Hamza Igamane alitoka kwenye benchi na kufunga bao lake la kwanza la kimataifa kutokana na kona iliyopigwa vyema kabla ya Azzedine Ounahi kukamilisha kipigo hicho.

    Ilikuwa jioni nzuri kwa Morocco walipocheza mechi ya kwanza katika Uwanja ulioboreshwa wa Prince Moulay Abdellah, ambao utaandaa fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika 2025 Januari ijayo na kutumiwa wakati ufalme huo utakapoandaa pamoja Kombe la Dunia la 2030.

    Washindi wengine wanane wa makundi katika kufuzu kwa Afrika wamehakikishiwa kujiunga na Atlas Lions kwenye fainali za 2026, huku washindi wanne waliomaliza nafasi ya pili wakiingia katika mchujo wa kufuzu katika mashindano ya mabara.

  7. Trump: Vita vya Ukraine vitaisha au tutalazimika kulipia gharama kubwa

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Rais Donald Trump

    Katika kikao kifupi katika Ikulu ya White House, Rais wa Marekani Donald Trump kwa mara nyingine amekiri kwamba kumaliza vita nchini Ukraine kumegeuka kuwa jambo gumu zaidi kuliko alivyofikiria.

    Trump alisema tayari alikuwa amemaliza vita saba na mzozo wa Ukraine utakabiliwa na "njia hiyo hiyo": "Lakini iligeuka kuwa ngumu zaidi kuliko nilivyofikiria," alisema.

    Lakini ikiwa vita havitaisha, "kutakuwa na gharama ya juu kulipa," Trump aliongeza, bila kutaja alichomaanisha.

    Trump alirejea Ikulu ya White House akiahidi kumaliza vita nchini Ukraine ndani ya saa zake 24 za kwanza madarakani. Tangu wakati huo amekiri kwamba mkataba wa amani si rahisi kupatikana.

  8. "Unaweza kuja Kyiv": Zelensky amjibu Putin kuhusu pendekezo la lake la kufanya mazungumzo Moscow

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Rais Putin wa Urusi na mwenzake wa Ukraine Volodymir Zelensky

    Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, katika mahojiano na ABC News, amekataa tena pendekezo la Rais wa Urusi Vladimir Putin kwenda Moscow kwa mazungumzo ya amani.

    "Anaweza kuja Kiev," Zelensky alisema. "Siwezi kwenda Moscow wakati nchi yangu inakabiliwa na mashambulizi ya makombora kila siku. Siwezi kwenda kwenye mji mkuu wa gaidi huyu," rais wa Ukraine aliongeza.

    Zelensky, akisisitiza juu ya mazungumzo katika ngazi ya wakuu wa nchi, amerudia kusema kwamba Putin hataki kukutana naye, kwani anaendelea kufanya vita nchini Ukraine.

    Siku ya Jumatano, baada ya ziara nchini Uchina, rais wa Urusi alisema kwamba "ikiwa Zelensky yuko tayari, aje Moscow." Zelensky alijibu Alhamisi huko Paris, ambapo alikuwa kwenye mkutano wa kilele wa "muungano wa walio tayari."

    "Nadhani ikiwa unataka mkutano usifanyike, unapaswa kunialika Moscow. Nadhani kwamba Urusi imeanza kuzungumza juu ya mkutano - hiyo tayari si mbaya. Lakini hadi sasa hatuoni nia yao ya kumaliza vita," rais wa Ukraine alisema.

    Putin aliendelea kusisitiza mjini Vladivostok siku ya Ijumaa kwamba Moscow ndiyo chaguo pekee la mazungumzo.

    "Sikiliza, upande wa Ukraine unataka mkutano huu na unapendekeza mkutano huu. Nilisema: Niko tayari, tafadhali njoo, kwa hakika tutatoa masharti ya kazi na usalama, dhamana ya 100%," rais wa Urusi alisema. "Ninarudia tena: ikiwa mtu anataka kweli kukutana nasi, tuko tayari. Mahali pazuri zaidi kwa hili ni mji mkuu wa Shirikisho la Urusi, jiji la shujaa la Moscow."

  9. Natumai hujambo