Sesko na Lammens waruhusu Man Utd kuwa na ndoto ya kuingia Ligi ya Mabingwa

Chanzo cha picha, Getty Images
Benjamin Sesko alikuwa mchezaji wa akiba wa Manchester United kwa mechi ya pili mfululizo huku Mslovenia huyo akifunga bao pekee dhidi ya Everton na kuwaweka vijana wa Michael Carrick katika nafasi ya nne.
Siku kumi na tatu baada ya mshambuliaji huyo wa pauni milioni 73.7 kufunga bao katika dakika za majeruhi na kuokoa pointi moja dhidi ya West.
Sesko aliendelea kutamba baada ya kumpa pasi Matheus Cunha. Kufikia wakati Cunha alipompa pasi ndefu Bryan Mbeumo, Sesko mwenye hamu kubwa alikuwa amewazidi nguvu walinzi wa Everton na alikuwa tayari kufunga bao lake la nane msimu huu.
Cha kushangaza, mabao mawili tu kati ya hayo yalifungwa na kocha wa zamani Ruben Amorim, huku matatu yakifungwa na Darren Fletcher katika michezo miwili akiwa kama kocha wa muda na matatu chini ya Carrick, ambaye sasa ameshinda michezo mitano kati ya sita aliyocheza akiwa kama meneja.
Ilikuwa wakati wa kusisimua baada ya muda mrefu katika mechi ambayo ilikuwa na ubora wa chini katika Uwanja wa Hill Dickinson.
Pande zote mbili zilipambana dhidi ya ulinzi mkali, baada ya kukaa kwa karibu wiki mbili bila mchezo baada ya kucheza mapema katika raundi ya mwisho ya mechi, mechi hii ikiwa mwishoni, na bila mechi yoyote katika Kombe la FA baada ya kutolewa mapema.
Katika mchezo wenye fursa finyu, mlinzi James Tarkowski alifanikiwa kuzuia mpira kuvuka mstari wa lango katika kipindi cha kwanza baada ya juhudi za Amad kuokolewa kiasi na Jordan Pickford.
Kipa Senne Lammens alimnyima kinda Harrison Armstrong, ambaye alikuwa na mchezo mzuri upande wa Everton kabla ya Michael Keane kuachia mpira kwa nguvu dakika nane kabla ya mpira kuisha.
Mpira ulikuwa unaelekea kwenye kona ya juu kushoto lakini Lammens alikuwa macho tena, huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji akiokoa mpira kwa njia ya kipekee.
Matokeo haya yanamaanisha kuwa sasa ni michezo saba ya nyumbani bila ushindi katika mashindano yote kwa Everton, ambao wako katika nafasi ya tisa.
Soma zaidi:



