Ushuru mpya wa Trump wa 10% waanza kutekelezwa
Ushuru mpya wa kimataifa wa Rais wa Marekani Donald Trump umeanza kutekelezwa kwa 10% baada ya Mahakama ya Juu Zaidi nchini humo kuzuia ushuru mkubwa wa uagizaji bidhaa siku ya Ijumaa.
Saa chache tu baada ya uamuzi wa wiki iliyopita, rais alisaini amri ya serikali ya kutoza ushuru mpya kuanzia tarehe 24 Februari.
Baadaye alitishia kuongeza ushuru huo hadi 15% lakini bado hajatoa agizo rasmi la kuongeza kiwango hicho. BBC imewasiliana na Ikulu ya White House kwa maoni.
Utawala unatekeleza hatu hii ya kuongeza ushuru chini ya Kifungu cha 122 cha Sheria ya Biashara ya 1974, ambayo inaruhusu rais kutoza ada hiyo kwa siku 150 bila idhini ya bunge.
"Nadhani inaongeza tu msukosuko," alisema Carsten Brzeski, mchambuzi wa benki ya uwekezaji ING, akimaanisha ushuru unaobadilika haraka na athari zake kibiashara.
"Kuhusu kutokuwa na uhakika tumerudi mahali tulipokuwa mwaka jana," aliambia kipindi cha BBC Today programme, akiongeza kuwa sasa kuna hatari kubwa zaidi kwamba washirika wa kibiashara wa Marekani watalipiza kisasi.
"Hatari ya vita kamili vya ushuru - vita vya kibiashara – iko uko juu zaidi kuliko mwaka jana," Brzeski alisema.
Soma zaidi: