Marekani yaituhumu Rwanda kukiuka mkataba wa amani Mashariki mwa DRC

Chanzo cha picha, Getty Images
Waziri wa Mambo ya kigeni wa Marekani, Marco Rubio, amesema kuwa hatua za Rwanda katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya demokrasia ya Congo (DRC) zinakiuka makubaliano ya amani yaliyosimamiwa na Rais Donald Trump.
Amesema hatua zitachukuliwa kuhakikisha kuwa ahadi zilizotolewa chini ya makubaliano hayo zinaheshimiwa.
Kwa upande wake, Rwanda imeituhumu DRC kwa kupuuza usitishaji mapigano na kuendeleza mashambulizi yake ya kurejesha maeneo yanayodhibitiwa na waasi wa M23.
Waziri wa Mambo ya kigeni wa Rwanda, Olivier Nduhungirehe, ameonyesha kushangazwa na madai yakuishutumu Rwanda kwa mapigano mapya, akisema kuwa waasi wa M23 walikuwa wakijibu mashambulizi kutoka kwa majeshi ya Congo.
Kauli yake inajiri baada ya balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa kuituhumu Rwanda kwa kuchochea eneo la Maziwa Makuu kuelekea vitani.
Waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda wameudhibiti mji wa pili kwa ukubwa katika jimbo la Kivu Kusini, karibu na mpaka wa Burundi.
Umoja wa Mataifa unasema kuwa ghasia za hivi karibuni zimesababisha zaidi ya watu laki mbili kuhama makazi yao.
Soma zaidi:






