Marekani yalegeza vikwazo dhidi ya ununuzi wa mafuta ya Urusi

Chanzo cha picha, Reuters
Bei ya mafuta ilipanda hadi zaidi ya $100 kwa pipa siku ya Alhamisi kutokana na mzozo unaoendelea, ikiwa ni pamoja na vitisho vya kusafirishwa kwa meli katika Mlango-Bahari wa Hormuz, njia yenye shughuli nyingi zaidi za usafirishaji wa mafuta duniani.
Marekani imelegeza vikwazo dhidi ya ununuzi wa mafuta ya Urusi na mafuta ya petroli ambayo tayari yamepakiwa kwenye meli baharini, ili kujaribu kupunguza athari za kiuchumi duniani.
Katibu wa Hazina Scott Bessent alisema msamaha huo wa muda wa siku 30 "hautaipatia serikali ya Urusi manufaa makubwa ya kifedha", ambayo ilisema ina takriban mapipa milioni 100 ya mafuta yanayosafirishwa kwa sasa.
Kremlin ilifuatia habari hiyo na kusema Urusi inaona hatua za Marekani kama "kujaribu kuleta utulivu katika masoko ya nishati" na kwa hivyo maslahi ya nchi zote mbili yanawiana.
Lakini waziri wa nishati wa Uingereza Michael Shanks aliambia BBC mapema kwamba Uingereza haitalegeza vikwazo dhidi ya mafuta ya Urusi "kabisa", akionya Vladimir Putin atapata fursa ya kuwekeza zaidi katika vita vya Ukraine.












