Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Moja kwa moja, Sitairuhusu Iran kuwa na silaha za nyuklia – Trump

Rais wa Marekani amesema: "Kwa miongo kadhaa, imekuwa sera ya Marekani kutoruhusu Iran kupata silaha za nyuklia.”

Muhtasari

Moja kwa moja

Rashid Abdallah

  1. Waziri Mkuu wa Senegal apendekeza sheria kali dhidi ya wapenzi wa jinsia moja

    Waziri Mkuu wa Senegal Ousmane Sonko amependekeza sheria ambayo inaweza kuongeza maradufu adhabu kwa watu wenye kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja, na kuwafanya waadhibiwe kwa hadi miaka 10 jela.

    Pendekezo hilo lilipelekwa bungeni Jumanne baada ya kuidhinishwa na baraza la mawaziri wiki iliyopita, baada ya wimbi la kukamatwa kwa watu wanaodaiwa kuwa wapenzi wa jinsia moja.

    Akihutubia wabunge, Sonko alisema muswada huo utaadhibu kile kinachoelezwa kama "vitendo kinyume na maumbile" kwa vifungo vya gerezani kuanzia miaka mitano hadi 10, ikilinganishwa na adhabu ya sasa ya mwaka mmoja hadi mitano.

    "Ikiwa kitendo hiki kitafanywa kwa mtoto mdogo, adhabu itakuwa ya juu zaidi," alisema, akikosolewa na watetezi wa haki za binadamu.

    Mjadala kuhusu haki za LGBT umesababisha mvutano kwa muda mrefu nchini Senegal, nchi ya kihafidhina ambapo baadhi ya makundi yanasema harakati za LGBT ni uingiliaji kati wa kigeni.

    Mashirika ya kidini yamekuwa yakifanya maandamano katika miaka ya hivi karibuni yakitaka adhabu kali zaidi.

    Mapema mwezi huu, polisi waliwakamata wanaume 12 chini ya sheria zinazopinga LGBT. Vyombo vya habari vya ndani vinasema takriban watu 30 wamekamatwa kwa jumla mwezi huu.

    Wale watakaopatikana na hatia wanaweza pia kukabiliwa na faini ya hadi CFA milioni 10 (karibu $18,000; £13,000), Sonko aliongeza.

    Tarehe bado haijawekwa kwa ajili ya kura ya bunge kuhusu muswada huo, katika bunge linalodhibitiwa na chama cha Sonko cha Pastef.

  2. Japan kupeleka makombora kwenye kisiwa karibu na Taiwan

    Waziri wa ulinzi wa Japani amesema anapanga kupeleka makombora kwenye kisiwa chake cha magharibi karibu na Taiwan ifikapo Machi 2031, huku mvutano wa kikanda ukiendelea.

    Ni mara ya kwanza kwa Japani kubainisha ratiba ya kupelekwa kwa kombora katika kisiwa cha Yonaguni.

    Yonaguni iko umbali wa kilomita 110 tu (maili 68) kutoka Taiwan.

    Mvutano kati ya Tokyo na Beijing umekuwa mkubwa tangu Novemba wakati Waziri Mkuu wa Japani Sanae Takaichi alipopendekeza kwamba Japani itakuwa tayari kujilinda iwapo kutakuwa na shambulio dhidi ya Taiwan.

    Wasiwasi ni kwamba shambulio lolote dhidi ya Taiwan, ambayo ni mshirika wa Marekani, linaweza kusababisha mzozo wa moja kwa moja wa kijeshi kati ya Washington na Beijing, kisha likaenea hadi kujumuisha washirika wengine wa Marekani katika eneo hilo kama vile Japani.

    Waziri wa ulinzi wa Japan Shinjiro Koizumi alitangaza ratiba ya makombora hayo siku ya Jumanne, siku moja baada ya China kuweka vikwazo vya usafirishaji nje kwa makampuni na mashirika 20 ya Japani.

    Koizumi alisema kitengo cha Yonaguni kitakuwa na makombora ya masafa ya kati yanayoweza kuzuia ndege na makombora.

    Matukio ya hivi punde yanakuja baada ya Takaichi, mhafidhina, kupata ushindi mkubwa katika uchaguzi wa bunge mapema mwezi huu.

    Ushindi huo ulimpa Takaichi nafasi ya kisiasa ya kuongeza nguvu katika kuimarisha uwezo wa ulinzi wa Japani.

    Pia unaweza kusoma:

  3. Kansela wa Ujerumani awasili Beijing kwa ziara ya kwanza nchini China

    Kansela wa Ujerumani amewasili nchini China huku uagizaji bidhaa kutoka China kwenda Ujerumani ulikuwa mara mbili ya bidhaa zilizosafirishwa mwaka jana kwenda Ujerumani - kulingana na takwimu za serikali kuu.

    "Tunataka ushirikiano na China ambao ni wa usawa, wa kuaminika, unaodhibitiwa na wa haki," amesema Friedrich Merz, kabla ya kuondoka kwenda Beijing.

    Kuna pengo kubwa la kibiashara linaonekana katika mazungumzo haya huku kansela akiongozana na ujumbe mkubwa wa kibiashara.

    Merz pia anatarajiwa kuishinikiza China kutumia ushawishi wake na Moscow kusaidia kukomesha vita nchini Ukraine.

    China kwa mara nyingine tena ilichukua nafasi ya kwanza kama mshirika mkubwa wa kibiashara wa Ujerumani 2025, ikichukua nafasi ya Marekani.

    Mnamo 2025, bidhaa zenye thamani ya €170.6 bilioni (£148.8bn; $200.9bn) zilitoka China hadi Ujerumani - ongezeko la 8.8% kila mwaka - huku mauzo ya nje ya Ujerumani kwenda China yakishuka kwa 9.7% hadi €81.3 bilioni .

    Uhusiano wa kibiashara na China upo zaidi katika sekta za magari, mashine na kemikali.

    Pia unaweza kusoma:

  4. Mafuriko na maporomoko ya ardhi Brazil yaua watu 25

    Watu wasiopungua 25 wamefariki katika jimbo la Minas Gerais kusini-mashariki mwa Brazil baada ya mvua kubwa iliyonyesha Jumatatu jioni kusababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi.

    Vifo vingi viliripotiwa katika jiji la Juiz de Fora, ambapo maafisa wanasema watu 18 walifariki, huku vifo vingine saba vikiripotiwa huko Ubá.

    Shughuli za uokoaji zinaendelea, huku wafanyakazi na wakazi wakiwatafuta watu walioripotiwa kupotea baada ya nyumba na majengo kadhaa kuanguka.

    Rais wa Brazil Luiz Inácio Lula da Silva alituma "rambirambi zake" kwa familia za waathiriwa na wale waliopoteza makazi yao. Pia alisema serikali imetangaza "hali ya janga" huko Juiz de Fora.

    Takriban watu 440 wameachwa bila makazi au wamelazimika kuhama makazi yao huko Juiz de Fora pekee, huku serikali ya mtaa ikitoa makazi ya muda na kuomba michango ya maji, chakula, nguo na vifaa vya usafi.

    Watoto walikuwa miongoni mwa wale waliofariki huko Juiz de Fora, lakini jiji hilo hadi sasa halijatoa taarifa yoyote rasmi kuhusu utambulisho wa waathiriwa.

    Pia unaweza kusoma:

  5. Sitairuhusu Iran kuwa na silaha za nyuklia – Trump

    Rais wa Marekani Donald Trump ametoa hotuba yake ya kila mwaka katika majengo ya Bunge la Marekani na kusisitiza kuwa hatoiruhusu Iran kuwa na silaha za nyuklia.

    Rais wa Marekani amesema: "Kwa miongo kadhaa, imekuwa sera ya Marekani kutoruhusu Iran kupata silaha za nyuklia.”

    “Wameonywa wasijaribu kujenga upya mpango wao wa silaha, lakini wanaendelea kufuata matarajio yao mabaya ya nyuklia. Napenda tutatue tatizo hili kupitia diplomasia, lakini jambo moja ni hakika: Sitawaruhusu kupata silaha za nyuklia."

    Trump ameweka rekodi ya hotuba ndefu zaidi, akitumia karibu saa 1 na dakika 50, akiizidi rekodi ya Bill Clinton ya hotuba yake ya mwisho mwaka 2000.

    Pia unaweza kusoma:

  6. 'Iwapo Marekani itafanya makosa ya kutushambulia itapata hasara kubwa' - Mkuu wa Jeshi Iran

    Hapo awali tuliripoti kwamba Waziri wa Ulinzi wa Armenia Soren Papikyan alisafiri hadi Tehran na kukutana na Waziri wa Ulinzi wa Irani Aziz Nasirzadeh.

    Meja Jenerali Abdolrahim Mousavi, Mkuu wa Jeshi la Iran pia alikutana naye.

    Bwana Mousavi alisema katika mkutano huo: "Sisi hatukuwa waanzilishi wa vita vyovyote, na mbinu yetu huko nyuma ilikuwa kuzuia kupanuka kwa wigo wa vita na kupunguza majeruha. Lakini hatua za Marekani zilitufanya kubadili mtazamo wetu, na wakati huu, ikiwa itafanya makosa, tutaisababishia hasara kubwa."

    Msemaji wa Ikulu ya White House Carolyn Leavitt amesema leo kuwa chaguo la kwanza la Donald Trump siku zote ni diplomasia, lakini yuko tayari kutumia nguvu ikibidi.

  7. Nigeria yakana ripoti kwamba ililipa fidia ili wanafunzi waliotekwa nyara waachiliwe huru

    Serikali ya Nigeria imekataa ripoti ya vyombo vya habari inayodai kwamba ililipa fidia kwa wanamgambo wa Kiislamu wa Boko Haram ili kuachiliwa huru kwa zaidi ya wanafunzi 200 na wafanyakazi waliotekwa nyara katika shule ya bweni ya Kikatoliki mwezi Novemba.

    Waziri wa Habari Mohammed Idris amesema madai hayo, yaliyotolewa na shirika la habari la AFP likinukuu vyanzo vya kijasusi, kuwa "ya uwongo na yasiyo na msingi."

    Pia amekanusha kwamba makamanda wawili wa Boko Haram waliachiliwa huru kama sehemu ya makubaliano hayo.

    Nigeria inakabiliwa na tatizo la utekaji nyara - huku wahalifu wakiwa ni pamoja na wanamgambo wa Kiislamu, wanachama wa magenge yanayojulikana kama "majambazi" na watu wanaotaka kujitenga.

    Baadhi ya wachambuzi walionukuliwa na AFP wanaamini utekaji nyara katika Shule ya St Mary huko Papiri katika jimbo la magharibi mwa Niger uliongozwa na kamanda maarufu wa wanamgambo wa Boko Haram anayejulikana kama "Sadiku."

    Ingawa Boko Haram inasalia kuwa na shughuli nyingi zaidi katika jimbo la Borno kaskazini-mashariki, ambapo kundi hilo lilianza uasi wake mwaka 2009, mitandao mingine ya uhalifu ina shughuli katika sehemu kubwa za maeneo ya kaskazini-magharibi na kaskazini-kati mwa Nigeria.

    Chanzo kimoja kilichonukuliwa na AFP kilidai fidia hiyo ilifikia takriban naira milioni 40 (karibu dola 30,000, pauni 22,000) kwa kila mateka, huku chanzo kingine kikidokeza kwamba jumla ya naira bilioni 2 (karibu dola milioni 1.5) zililipwa.

    Ripoti hiyo pia ilidai pesa hizo zilisafirishwa kwa helikopta hadi kwenye eneo la Gwoza la Boko Haram katika jimbo la Borno na kukabidhiwa kwa kamanda wa eneo hilo.

    "Madai kwamba fidia ilitolewa kwa helikopta kwa waasi, pamoja na uthibitisho wa risiti, ni hadithi ya kubuni," Idris alisema katika taarifa hiyo.

    Boko Haram walipata umaarufu mwaka 2014 kwa kuwateka nyara zaidi ya wasichana 200 wa shule kutoka kijiji cha Chibok.

    Tangu wakati huo nchi imekabiliwa na ongezeko la utekaji nyara kwa wingi, huku wachambuzi wakisema malipo ya fidia - kutoka kwa familia, wapatanishi au, katika baadhi ya matukio, mamlaka za serikali - yamesaidia kuchochea utekaji nyara."

    Pia unaweza kusoma:

  8. Mexico yawasaka wafungwa 23 waliotoroka gerezani wakati wa vurugu

    Polisi nchini Mexico inawasaka wafungwa kadhaa waliotoka gerezani huko Puerto Vallarta wakati wa wimbi la machafuko yaliyoanzishwa na genge la dawa za kulevya la Jalisco New Generation Cartel (CJNG) siku ya Jumapili.

    CJGN ilifanya vurugu kulipiza kisasi kwa mauaji ya kiongozi wao, Nemesio Oseguera Cervantes, anayejulikana kama "El Mencho" na vikosi vya usalama.

    Wakati wa machafuko hayo, watu wenye silaha waligonga milango ya gereza kwa gari, na kuwafungulia njia wafungwa 23 kutoroka, amesema afisa mmoja.

    Zaidi ya watu 70 - wakiwemo wanajeshi 25 - waliuawa katika operesheni ya kukamata El Mencho na vurugu zilizofuata.

    Pia unaweza kusoma:

  9. Hujambo na karibu

    Nakukaribisha katika taarifa zetu za moja kwa moja, leo Jumatano tarehe 25/2/2025