Je Taiwan inaweza kujitetea katika vita dhidi ya China?

Wiki iliyopita, ndege tano za kivita za China zilivuka tena mpaka wa Taiwan.

Rais wa Marekani Joe Biden amesema yuko tayari kutumia nguvu kulinda Taiwan, lakini maafisa wa Ikulu ya White House wanasisitiza kuwa Marekani hijabadili msimamo wake.

Washington imekuwa na sera ya muda mrefu ya "utata wa kimkakati" kuhusu suala la kuingilia kijeshi katika tukio la shambulio la China dhidi ya Taiwan.

Rais Xi Jinping wa China amesema "kuungana tena" na Taiwan "lazima kutekelezwe" - na hajapinga uwezekano wa matumizi ya nguvu kufanikisha hili.

China inachukulia Taiwan inayojitawala kama jimbo lililojitenga ambalo hatimaye litakuwa sehemu ya nchi hiyo tena.

Hata hivyo, Taiwan inajiona kama nchi huru, yenye katiba yake na viongozi waliochaguliwa kidemokrasia.

Taiwan ni wapi?

Taiwan ni kisiwa, kilichopo karibu maili 100 kutoka pwani ya kusini mashariki mwa China.

Map of China and Taiwan with neighbouring states..

Ipo katika kile kinachojulikana kama "mlolongo wa kisiwa cha kwanza", ambayo inajumuisha orodha ya maeneo kadhaa yaliyo na uhusiano wa kirafiki na Marekani na ni muhimu kati sera ya kigeni ya nchi hiyo.

Iwapo Uchina itachukua mamlaka ya Taiwan, baadhi ya wataalam wa nchi za magharibi wanapendekeza kuwa inaweza kuwa huru zaidi kupanga nguvu katika eneo la magharibi mwa Pasifiki na inaweza hata kutishia kambi za kijeshi za Marekani zilizo mbali kama Guam na Hawaii.

Lakini China inasisitiza kuwa nia yake ni ya amani tu.

Kwa nini kuna utata kuhusu Taiwan?

China inaamini kwamba Taiwan ni moja ya majimbo yake, ambayo siku moja itakuwa sehemu ya China.

Taiwan, kwa upande mwingine, inajiona kuwa nchi huru, ina katiba yake na inaongozwa na serikali iliyochaguliwa na wananchi.

Taiwan ni kisiwa kilicho umbali wa maili 100 kutoka pwani ya kusini mashariki mwa Uchina.

Iko eneo ambalo nchi nyingi zinazounga Marekani mkono ziko.

Visiwa hivi vyote ni muhimu sana kwa sera za nje ya Marekani.

Iwapo China itaichukua Taiwan, itakuwa huru kuendeleza utawala wake magharibi mwa bahari ya Pasifiki, kwa maoni ya wataalamu wengi wa nchi za Magharibi.

Baada ya hapo kambi ya kijeshi ya Marekani huko Guam na visiwa vya Hawaii pia vinaweza kuwa hatarini.

Hata hivyo, China inadai kwamba nia yake ni ya amani.

Marais Putin na Xi jingpin

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Marais Putin na Xi jingpin

Kwa nini Taiwan ilijitenga na Uchina?

Kutengena kati ya wawili hawa kulitokea baada ya Vita ya pili ya Dunia.

Wakati huo, Chama cha Kikomyunisti cha China katika China Bara kilikuwa kinapigana na Chama tawala cha Nationalist au Kuomintang.

Mwaka 1949, Chama cha Kikomunisti cha China kikiongozwa na Mao Zedong kilishinda na kuuteka mji mkuu wa Beijing.

Baada ya hapo, watu wa Kuomintang walikimbia bara hadi kisiwa cha Taiwan.

Tangu wakati huo, Kuomintang kimesalia kuwa chama muhimu zaidi nchini Taiwan. Kwa sehemu kubwa ya historia ya Taiwan, Chama cha Kuomintang kimetawala.

Hivi sasa, ni nchi 13 tu ulimwenguni zinazoitambua Taiwan kama nchi huru.

China ina shinikizo nyingi za kidiplomasia kwa nchi nyingine kutoitambua Taiwan.

Pia ni jitihada za China kwamba nchi nyingine hazipaswi kufanya jambo ambalo linaweza kuitambua Taiwan.

Waziri wa ulinzi wa Taiwan amesema uhusiano wake na China ni mbaya zaidi katika kipindi cha miaka 40 iliyopita.

Je, Taiwan inaweza kujitetea?

China inaweza kuiunganisha tena Taiwan hata kwa kuchukua hatua kando na mbinu za kijeshi.

Hili linaweza kufanywa kwa kuimarisha uhusiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo mbili.

Lakini ikiwa kuna vita kati ya nchi hizo mbili, basi nguvu ya kijeshi ya Taiwan itaonekana kuwa dhaifu mbele ya Uchina.

Matumizi ya kila mwaka ya China kwa jeshi lake ni ya juu zaidi ulimwenguni isipokuwa ya Marekani.

Nguvu zake za kijeshi ni tofauti kabisa na kubwa.

Hakuna nchi inyoikaribia China kwa ukubwa wa jeshi lake duniani
Maelezo ya picha, Hakuna nchi inyoikaribia China kwa ukubwa wa jeshi lake duniani

Je, hali inazidi kuwa mbaya?

Mnamo 2021, China ilionekana kuishinikiza Taiwan kwa kutuma ndege zake kwenda kwa mifumo ya eneo la ulinzi wa anga.

Eneo la ulinzi wa anga la nchi ni eneo ambalo ndege za kigeni hutambuliwa, kufuatiliwa na kudhibitiwa ili kulinda nchi.

Taiwan ilitoa data za kutumwa ndege hizo mnamo mwaka 2020.

Mnamo Oktoba 2021, ndege 56 za China ziliripotiwa kuingia katika eneo la Taiwan kwa siku moja.

Kwa nini Taiwan ni muhimu kwa ulimwengu?

Uchumi wa Taiwan una maana kubwa kwa ulimwengu.

Asilimia kubwa ya vifaa vinavyotumiwa kwenye vyombo vya kielektroniki duniani kama vile simu, kompyuta, saa na vifaa vya michezo vinatengenezwa Taiwan.

Kwa sasa Taiwan ndio hitaji kubwa zaidi ulimwenguni katika suala la vifaa hivyo. Chukua kwa mfano kampuni inayoitwa 'One Measure'.

Kampuni hii pekee inazalisha zaidi ya nusu ya vifaa vya 'chips' duniani.

Sekta ya vifaa hivi duniani ilikuwa na thamani ya takriban $100 bilioni mwaka 2021 na inaongozwa na Taiwan.

Ikiwa Taiwan itachukuliwa na Uchina, basi Uchina itakuwa na udhibiti wa sekta muhimu kama hiyo ya ulimwengu.

Je! watu wa Taiwan wana wasiwasi?

Licha ya kuongezeka kwa mvutano kati ya China na Taiwan, utafiti wa hivi karibuni unaonyesha kuwa haujawa na athari kubwa kwa watu nchini Taiwan.

Mnamo Oktoba, Wakfu wa Maoni ya Umma wa Taiwan uliuliza watu kama wanafikiri vita na China vitatokea. Takriban asilimia 64 ya watu wa Taiwan walijibu 'hapana' .

Wakati huo huo, utafiti mwingine ulionyesha kuwa watu wengi wa Taiwan wanajiona tofauti na watu wa China.

Uchunguzi uliofanywa na Chuo Kikuu cha cha Chengchi uligundua kwamba utambulisho wa UTaiwan miongoni mwa watu nchini Taiwan umeongezeka ikilinganishwa na mwaka 1990.

Mwelekeo wa watu kujiona kuwa Wachina au WaTaiwan na Wachina umepungua sana.