Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kenya: Maafisa 8 wa polisi wauawa katika mlipuko wa bomu Wajir
Maafisa wanane wa polisi wanahofiwa kufariki baada ya gari la polisi lililokuwa likipiga doria mjini Wajir Kaskazni mwa Kenya kukanyaga bomu.
Inspekata jenerali a polisi Hillary Mutyambai ametoa taarifa iliosema kuwa gari hilo llikuwa imewabeba maafisa 11 na ilikuwa ikipiga doria katika mpaka wa Kenya na Somalia.
Tayari vikosi vya usalama ikiwemo wale wa anagni wamepelekwa katika eneo hilo kufuatia kisa hicho.