Brexit: Theresa May kujiuzulu kama Waziri Mkuu Uingereza Juni 7

Chanzo cha picha, Reuters
Theresa May kujiuzulu kama kiongozi wa chama cha Conservative tarehe 7 Juni na kutoa fursa kuidhinishwa mchakato wa kuchaguliwa waziri mkuu mpya Uingereza.
Katika taarifa iliojaa hisia alioitoa huko Downing Street, Bi May amesema amefanya "kila awezalo" kutekeleza matokeo ya kura ya maoni kuhusu EU ya mnamo 2016.
Ni jambo linalosalia kuwa "na majuto mengi" kwamba ameshindwa kutimiza Brexit - Uingereza kujitoa katika Umoja wa Ulaya, ameongeza.
Lakini waziri mkuu mpya ndio suluhu " kwa manufaa ya taifa".
Bi May amesema ataendelea kuhudumu kama waziri mkuu wakati kukitarajiwa kuidhinishwa mchakato wa kumchagua kiongozi mpya wa chama cha Conservative.
Atajiuzulu kama kiongozi wa chama hicho Juni 7 na uteuzi wa waziri mkuu mpya unatarajiwa kuanza wiki inayoafuata baada ya hatua hiyo.
Miaka 3 ahudumu kama waziri baada ya kuondoka David Cameron
Miaka 6 kabla ya hapo, waziri wa mambo ya ndani
Ashindwakatika uchaguzi mkuu 2017 , lakini asalia waziri mkuu
Asaliampiga kura katika kura ya maoni ya EU mnamo 2016
Brexit iligubika muda aliohudumu 10 Downing Street
Sauti yake ilittereka na alikuwa mwingi wa hisia alipomaliza hotuba yake akisema: "Nitaondoka katika wadhifa huu hivi karibuni lakini imekuwa heshima kubwa maihsani mwangu kuhudumu.
"Waziri mkuu mwanamke wa pili, na bila shaka sio wa mwisho.
"Nachukua hatua hii bila ya uovu wowote, bali na shukrani za dhati na kubwa kutokana na kupata fursa kuitumikia nchi ninayoipenda."














