Kwa Picha: Mwezi mwekundu ulivyoonekana kote duniani

Watu katika mataifa mengi dunia walifanikiwa kutaza kupatwa kwa mwezi uliobadilika na kuwa mwekundu ikiwa ni tukio la muda mrefu la aina yake katika karne ya 21.

Nchini Ugiriki, mwezi ulipanda nyuma ya hekalu la Poseidon mjini Cape Sounion, karibu na mji mkuu wa Athens.

Katika tukio la kupatwa kwa mwezi, dunia kuwa katikati ya mwezi na jua

Ijapokuwa hupata mwangaza moja kwa moja kutoka kwa Jua, mwezi huo ulikuwa ukipata mwanga kidogo unaotokana na kuinama kwa mbingu ya dunia.

Hatua hiyo unaipatia mwezi huo rangi ya machungwa, kahawa au nyekundu.

Mwezi huo ulionekana kutoka Afrika hadi Mashariki ya Kati, Ulaya, Urusi, India na Australia.

Mjini Strasbourg, Ufaransa, mwezi ulionekana ukipitia juu ya sanamu hii iliochongwa na msanii wa Marekani Jonathan Borofsky.

Nchini Uswizi uliweza kuonekana juu ya kilele cha milima ya Alps

Watu waliokuwa wakiutizama hawakuhitaji kifaa chochote ili kuuona mwezi huo.

Huku mwezi huo iukipita juu ya Abu Dhabi, uliweza kuonekana katika mnara mrefu mwembamba wa msikiti mkubwa wa Sheikh Zayed .

Mjini Sydney, umati wa watu ulikusanyika ili kutazama Mwezi mwekundu katika u juu ya mbingu todauti za mji.

Watu huko Taipei, Taiwan, walianzisha vifaa vya teknolojia ili kutazama tukio hilo. kupatwa kwa mwezi kulichukua takriban saa moja na dakika 43.