Jamii Forums wafunga huduma Tanzania baada ya wanablogu wasio na leseni kuzuiwa kupakia taarifa

Jukwaa maarufu nchini Tanzania Jamii Forums limekuwa miongoni mwa watoaji huduma za maudhui mtandaoni ambao wameathiriwa na kuanza kutekelezwa kwa sheria mpya za mtandaoni.
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania imewataka watu ambao wamekuwa wakitoa imetoa ilani kwa wahudumu wote ambao bado hawajapata leseni kukoma kutoa huduma hizo kuanzia leo.
Mamlaka hiyo imesema wahudumu hao wana hadi Ijumaa wiki hii kuhakikisha wamejipatia leseni la sivyo watachukuliwa hatua.
TCRA imesema wanaoathirika ni wamiliki wote wa blogu, majukwaa ya mitandaoni, redio na televisheni.

Wameandika kwenye mtandao wao:
"Kutokana na notisi iliyotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) leo Juni 10, 2018 inayotoa muda mfupi wa kututaka kusitisha utoaji huduma mara kabla ya Juni 11, 2018, tunalazimika kutii mamlaka na hivyo huduma hii haitapatikana kwa muda wakati tukifanya jitihada za kuhakikisha huduma inarejea.
"Kwa wateja wetu walio nchi nyingine, huduma hii itarejea mapema zaidi lakini kwa walio Tanzania kurejea kwa huduma kutategemeana na matokeo ya hatma ya jitihada za wawakilishi wetu walio Tanzania.
"Tunasikitika kuwa tunalazimika kufikia hatua hii ghafla lakini ni matumaini yetu kuwa wateja wetu mtaendelea kuwa wavumilivu katika kipindi hiki."
Ujumbe wa mwisho kutoka kwa jukwaa hilo kwenye Twitter ulipakiwa usiku wa manane, na ulikuwa wa kutangaza taarifa hiyo kutoka kwa TCRA.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 1
Mwanablogu Carol Ndosi ni miongoni mwa walioathiriwa na kuanza kutekelezwa kwa sheria hizo, mwanzoni aliomba ufafanuzi kuhusu wanaotakiwa kusitisha kuchapisha taarifa mtandaoni.
Baadaye, aliandika kwamba amelazimika kusitisha uandishi wa taarifa mtandaoni.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 2
Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe ni miongoni mwa walioshangazwa na hatua ya sheria hiyo kuanza kutekelezwa na Jamii Forums kulazimika kufunga huduma zao kwa muda.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 3
Wamiliki wa huduma za mitandaoni Tanzania walikuwa wamepewa muda wa wiki mbili kujisajili baada ya serikali kushinda kesi iliofunguliwa na wadau wa habari kupinga kanuni za maudhui mitandaoni 2018.
Wanablogu ambao wataopatikana na hatia ya kutoheshimu sheria hizo mpya watakabiliwa na faini ya hadi milioni 5 ama kifungo kisichopungua miezi 12 ama zote mbili kulingana na sheria hizo mpya, ilisema taarifa hiyo.
Mike Mushi, mwanzilishi mwenza wa Jamii Forums alikuwa awali ameambia BBC kwamba kanuni hizo, ambazo zinawataka wachapishaji wa taarifa zenye maudhui mtandaoni kuhifadhi maelezo ya wachangiaji kwa miezi 12 huenda zikaathiri mtandao wa Jamii Forums.
"Sheria hizi zinaenda kinyume na jinsi sisi huendesha shughuli zetu. Huwa twawaruhusu watumiaji wetu kuandika ujumbe bila majina yao kutambulishwa, hivyo itatulazimu kufikiria kwa kina iwapo tutaweza kuendeleza kuendesha shughuli zetu."
Alisema mtandao huo kufikia Aprili ulikuwa na watumiaji 3.7 milioni kwa mwezi na walikuwa wanapokea ujumbe takriban 20,000 kila siku.

Rais Magufuli alitoa agizo la kumchukulia hatua kali za kisheria mtu yeyote atakayechapisha habari za uongozi kuhusu serikali katika mitandao ya kijamii.
Idadi ya watumiaji wa mitandao nchini Tanzania ilipanda hadi asilimia 16 (watu 23 milioni) mwaka 2017. Hiyo ni sawa na asilimia 44 ya raia wa Tanzania.
Wengi hutumia simu kupata huduma za mtandao.













