Mashindano ya urembo wa ngamia Saudi Arabia yatumbukia katika kashfa

A man cheers as he rides a camel during King Abdulaziz Camel Festival in Rimah Governorate, north-east of Riyadh, Saudi Arabia January 19, 2018

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Visitors to the festival in al-Dahna, north of Riyadh, can also watch camel racing

Ngamia 12 wamepoteza sifa za mashindano ya urembo nchini Saudi Arabia baada ya wamiliki wao kuwachoma sindano ya kubadili maumbile.

Maelfu ya ngamia wameshirikiswa katika tamasha la Mfalme Abdulaziz na kushindanishwa kwa muonekano wa nyuso zao, nundu na maumbile yao.

Lakini majaji waliingia kati wakati walipogundua kwamba baadhi ya udanganyifu ulifanyika na baadhi ya wamiliki waliotaka kushinda tuzo za fedha.

Saudi men stand next to camels as they participate in King Abdulaziz Camel Festival in Rimah Governorate, north-east of Riyadh, Saudi Arabia January 19, 2018

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Shindano lina vigezo vikali vya urembo

Vile vile tamasha hilo lina mashindano ya riadha ya ngamia na kuonja maziwa, lina tuzo ya fedha taslim dola milioni 57.

Mtandao wa habari wa The National imeripoti kuwa Ali Al Mazrouei, mwana wa mfugaji bingwa , alisema dawa ya botox ilitumika kwenye midomo, pua na hata taya.

"Dawa hiyo inavimbisha kichwa kwa hio ukimuona ngamia unadhani ana kichwa,mdomo na pua kubwa" aliezea Mazrouei.

A Saudi man walks in front of camels as he participates in the King Abdulaziz Camel Festival in Rimah Governorate, north-east of Riyadh, Saudi Arabia January 19, 2018

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Tamasha hilo linasherekea tamaduni za Kisaudia

Majaji pia walikuwa wakishindanisha nundu na misuli ya ngamia.

Kabla ya tamasha hilo, vyombo vya habari vya Saudia viliripoti daktari wa wanyama alikamatwa akiwa pasua ngamia hao ili kuwabadilisha ukubwa wa masikio pamoja na kuwachoma sindano ya dawa ya kubadilisha maumbile.

line

Pia unaweza soma yafuatayo

Jaji mkuu Fawzan al-Madi amesema kuwa ngamia ni moja wapo wa "nembo ya Saudi Arabi"

Mashindano hayo ya urembo wa ngamia yalifanyika kwa mara ya kwanza mwaka 2000.