Mwanafunzi aliyevaa hijab azuiwa kufuzu chuoni Nigeria

Chanzo cha picha, Alamy
Mwanafunzi wa sheria nchini Nigeria amazuiwa kufuzu baada ya yeye kusisitiza kuvaa hijab wakati wa sherehe za kufuzu.
Amasa Firdaus, ambaye alifuzu kutoka chuo cha Ilorin, alizuiwa kuingia ukumbi wa kufuzu kwenye mji mkuu Abuja ambapo sherehe zilikuwa zikifanyika.
Alikataa kuvua hijab yake akisitiza kuwa angevaa kofia ya kufuzu juu ya hijab yake.
Hii ilitajwa kuwa kuenda kinyume na vazi ramsi lililoweka na vyuo vya sheria.
Kesi hiyo imevutia husia kubwa katika mitandao ya kijamii.
Mtumiaji mmoja wa mtandao wa Instagram alisema kuwa Bi Firdaus ana haki ya kufanya hivyo.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa Instagram ujumbe








