Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Museveni: Kujiepusha na pombe kumechangia maisha marefu
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amefichua kwamba huwa hanywi pombe na kusema hilo limechangia maisha yake marefu.
Museveni, 73, ameandika kwenye Twitter kwamba uamuzi wake huo umemkinga dhidi ya maradhi na kusema kwamba hana "muda wowote wa magonjwa".
Wabunge nchini Uganda kwa sasa wanajadili mswada ambao unaondoa kikomo kwenye umri wa rais, ambacho kwa sasa ni miaka 75.
Sheria isipofanyiwa marekebisho na kikomo hicho kuondolewa, Bw Museveni hawezi kuruhusiwa kuwania kwa muhula wa sita uchaguzi wa mwaka 2021.