Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Nyusi kuwania tena urais Msumbiji 2019
Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi ameidhinishwa na chama tawala cha Frelimo kuwania tena urais nchini humo.
Uchaguzi mkuu nchini humo utafanyika mwaka 2019.
Alipochaguliwa mwaka 2015, Nyusi alipata asilimia 57 ya kura zilizopigwa na kumshinda mpinzani wake wa karibu Afonso Dhlakama, kiongozi wa chama cha upinzani cha National Resistance (Renamo).
Dhlakama alipata 37% ya kura zilizopigwa.
Renamo - ambao walipigana vita vya muda mrefu vya wenyewe kwa wenyewe dhidi ya Frelimo ambavyo vilifikia kikomo 1992 na kusababisha vifo vya watu zaidi ya milioni moja - walipinga matokeo hayo.
Licha ya ukuaji mzuri wa uchumi, zaidi ya nusu ya raia 24 wa Msumbiji wameendelea kuishi maisha ya ufukara.