Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ufaransa yapambana na moto wa msituni
Hali isiyotarajiwa ya upepo, joto na kiangazi kikali Kusini Mashariki mwa Ufaransa, imechangia kuenea kwa kasi kwa moto wa msituni, kote katika eneo hilo.
Wazima moto 600 wanakabiliana na moto huo ambao ulianza Jumatatu asubuhi, katika mbuga moja ya kitaifa ya wanyama pori, iliyoko katika jimbo la Luberon, na kufikia sasa moto huo unateketeza eneo la ukubwa wa kilomita 8 mraba.
Mamia ya watu wamehamishwa kama njia ya kuchukua tahadhari