Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Jeshi kusaidia kuzima moto mkubwa uliozuka msituni Canada
Maafisa katika jimbo la British Columbia nchini Canada wamesema wanaweza kuomba msaada kutoka jeshi la nchi hiyo kusaidia kuuzima moto mkubwa uliosababisha zaidi ya watu elfu saba kuyahama makazi yao.
Takriban wazimamoto elfu mbili wanapambana na moto huo uliozuka mwishoni mwa juma huku vikosi zaidi vikiongezwa.
Ndege za kuzimia moto pia zimetumwa kutoka mji wa jirani wa Saskatchewan.
Siku ya Jumamosi jimbo la British Columbia lilitangaza hali ya hatari kwa mara ya kwanza baada ya kipindi cha miaka 14 kutokana na moto huo.