Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Watu watatu wauawa kwa kupigwa risasi Marekani
Polisi katika mji wa San Francisco wamesema watu watatu wameuawa katika shambulio la kufyatua risasi.
Mfyatuaji ambaye alikuwa amevalia mavazi ya kampuni moja pia alifariki.
Polisi wanasema alijifyatulia risasi mwenyewe wakati wakijaribu kumkamata.
Watu wengine wawili walijeruhiwa katika shambulizi hilo.
Msemaji wa jeshi la polisi amesema kuwa tukio hilo halina uhusiano na ugaidi.