Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Vikosi vya Marekani vyaharibu ngome ya Al-Shabaab Somalia
Rais wa Somalia Mohammed Abdullahi Farmajo amesema moja ya ngome kubwa za wapiganaji wa Al-Shabaab zimeharibiwa vibaya baada ya shambulizi lililofanywa na vikosi vya Marekani.
Amesema kuwa vikosi maalum vya jeshi la Somalia vinavyopata mafunzo kutoka vile vya Marekani pia vilihusika kuwashambulia Al-Shabaab.
Vikosi vya Marekani vimethibitisha kufanya shambulizi hilo Kusini mwa Somalia.
Haijajulikana kama pametokea uharibifu mwingine wowote.
Siku ya Alhamisi vikosi vya Al-Shabaab viliua watu 59 katika shambulizi kwenye mji wa Puntland Kusini mwa Somalia.