Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Sera ya familia kuwa na watoto 2 yaleta mabadiliko China
Uchina inasema uamuzi wake wa kuruhusu familia kuwa na watoto wawili badala ya mmoja tu, umeleta mabadiliko thabiti.
Afisa wa upangaji uzazi , amesema watoto milioni 18 zaidi walizaliwa mwaka jana ikiwa ni milioni mbili zaidi kushinda miaka iliyopita.
Lakini mabadiliko hayo ya sera hiyo , hayatazuwia wananchi wa Uchina kwa jumla, kuwa wazee swala ambalo litasababisha wazee zaidi na raia wachache walipa kodi kuweza kuwasaidia hao wazee.
Pia watoto zaidi waliozaliwa siyo wengi kama wakuu walivyotaraji walipobadilisha sera hiyo mwaka wa 2015